.

.

.

.

Friday, November 27, 2015

KIMENUKA TRA


Raisi wa Tanzania, Dkt John Pombe Joseph Magufuli amemsimamisha kazi, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)Rished Bade kufuatia kasoro kubwa za kiutendaji zilizobainika katika Mamlaka ya Mapato nchini.

Rais amechukua uamuzi huo hii leo baada ya ziara ya kushtukiza ya Waziri Mkuu, Majaliwa Kasimu Majaliwa katika Bandarini jijini Dar es Salaam.

Kasoro hizo ni pamoja na na kuingizwa nchini kwa makontena zaidi ya 300 ambayo hayajalipiwa ushuru na hivyo kusababisha upotevu wa zaidi ya shilingi bilioni 80 za mapato ya serikali.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue,alisema kufuatia kusimamishwa kazi kwa bade, Rais amemteua Dk. Philip Mpango kuwa Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato (TRA).
 
Kabla ya uteuzi huo, Dk Mpango alikuwa Katibu Mtendaji wa tume ya Mipango.

Pamoja na hatua hizo Balozi sefue amsema Raios Magufuli ameagiza watu wote ambao wanajijua kuwa wameingiza nchini makontena ya bidhaa mbalimbalipasipo kulipa ushuru na kodi kama inavyopaswa waende wenyewe katika mamlaka ya Mapato Tanzania kulipa ushuru unaopaswa.

Wakati huohuo Balozi Sefue amesema safari zote zawafanyakazi wa TRA nje ya nchi zimefutwa kuanzia leo na badalayake amewataka hao kutoa ushirikiano wakati wa uchunguzi zaidi katika mamlaka hiyo ukiendelea.

No comments:

Post a Comment