Monday, 30 November 2009

CHADEMA NI SHWARI

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo na Demokrasia CHADEMA Freeman Mbowe amekanusha uvumi kuwa yeye na Naibu Katibu Mkuu wake Zitto Kabwe wana 'bifu' na hivyo hawaelewani, huku akitaka taarifa hizo zipuuzwe kwa vile hazina ukweli wowote.
Aidha, Mbowe amekanusha pia madai kuwa CHADEMA kina nia ya kumtimua Zitto na badala yake amesema kuwa Mbunge huyo wa Jimbo la Kigoma Kaskazini (Zitto) ni tegemeo katika chama na kamwe hakuna mpango wowote wa kumuengua.
“Nani anasema mimi nina ugomvi na Mheshimiwa Zitto... sina ugomvi wowote na Zitto. Yeye namchukulia kama kiongozi mwenzangu na mtu muhimu katika chama chetu,” amesema Mbowe.
Akaongeza kuwa CHADEMA kina kazi ngumu mbele ya kuendelea kujiimarisha na hakina muda wa kuanza kuendeleza ugomvi ambao haukijengi chama ila kukidhoofisha.
Akasema kama ni tofauti zilizokuwa wakati wa uchaguzi mkuu wa chama chao, hizo nd'o hazina nafasi kabisa ya kuwagawa kwani zilishamalizwa katika mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika miezi michache iliyopita Jijini Dar.
"Sisi kama viongozi, tulishikana mikono ili kumaliza tofauti zozote zilizokuwapo wakati wa uchaguzi,” akasema Mbowe.
Akizungumzia tuhuma zilizotolewa na viongozi walioondolewa katika nafasi zao hivi karibuni kuwa yeye kama mwenyekiti amekuwa akifuja ruzuku ya chama, akasema hawezi hata siku moja kula ruzuku hiyo, ambayo ni ndogo sana ukilinganisha na mahitaji halisi ya chama.
Akaongeza kuwa hivi sasa, chama chao kinaambulia kiasi cha shilingi milioni 60 kiwango ambacho ni kidogo sana ukilinganisha na majukumu makubwa yanayokikabili chama hicho kitaifa.
"Mimi kama Mwenyekiti silipwi mshahara wala posho na chama ... na wala sitaki kulipwa kwa sababu najua kazi kubwa iliyopo ni kukijenga zaidi chama,” amesema Mbowe.
Aidha, akasema kwa mujibu wa utaratibu, hakuna kiongozi hata mmoja anayeweza kuchukua fedha katika akaunti ya chama bila hicho bila wajumbe wengine kuhusishwa.
"Kwa utaratbu wetu, wanaotia saini ya kuchukua fedha katika akaunti ya chama ni mwenyikiti, katibu na Mkurugenzi wa fedha wa chama... sasa ni wapi ambapo mimi naweza kuchukua fedha za chama peke yangu... hakuna kitu kama hicho!" Akasema.
Kuhusiana na waliofukuzwa uongozi hivi karibuni, Mbowe amesema ni vyema watu wakaelewa kuwa waliondolewa si kisiasa bali kutokana na utendaji wao na siku zote walipaswa kuwajibika kwa katibu mkuu, kwa mujibu wa utaratibu wa CHADEMA.
“Mimi kama mwenyekiti wa chama, huwezi kunifananisha na hao waliofukuzwa kwa sababu mimi sikuteuliwa bali nimechaguliwa, tena na wajumbe wa mkutano mkuu,” amesema Mbowe.
CHANZO: ALASIRI

KAZI ZA MAPAPARAZI HIZI HAPA ....







UZALISHAJI WA CHUMA LUDEWA

Mwenyekiti wa bodi ya Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) Chrisant Mzindakaya akiangalia moja ya malighafi ya kuzalisha chuma katika Eneo la Liganga mkoani Iringa.. Kulia ni Waziri Kiongozi mstaafu wa Zanzibar ambaye ni mjumbe wa bodi hiyo Dk Gharib Bilal na katikati ni Katibu Tarafa wa Ludewa.

MAMA SALMA KIKWETE .....


Mama Salma Kikwete akikaribishwa kwa kukumbatiwa na Mke wa Waziri wa Trinidad na Tobago, Seneta Hazel Manning wakati Mama Kikwete alipowasili kwenye Kituo cha Kidiplomasia mjini Port of Spain kuhudhuria Kongamano la Wajasiriamali lililoandaliwa nchini humo, Jumamosi, Novemba 28, 2009, na Seneta huyo kama sehemu ya shughuli za wake wa wakuu wa Serikali wanaohudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuia ya Madola. (Picha na Juma Kengele, Ikulu)

MAFUA YA NGURUWE MKOANI MWANZA

SERIKALI mkoani Mwanza imezifunga shule za msingi 150 na sekondari 27 wilayani Kwimba ili kuzuia kusambaa kwa ugonjwa wa mafua ya nguruwe ambao mpaka sasa umeathiri watu 221 wilayani humo.
Akizungumza wakati wa kutoa taarifa ya wilaya kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Abbasi Kandoro aliyetembelea shule ya msingi Ilula jana, Mkuu wa Wilaya ya Kwimba, Ryoba Christopher Kangoye alisema uamuzi huo umechukuliwa ili kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huo wilayani humo.
Alisema uamuzi wa kufunga shule hizo umeenda sambamba na kupiga marufuku minada na mgulio yote wilayani humo.
Tumeamua kufunga shule hizo kabla ya muda wake kwa sababu wanafunzi wanatoka nyumbani na kuja shuleni kila siku. Hali hii inaweza kuchangia kuongeza kasi ya mlipuko wa ugonjwa wa homa ya mafua ya Nguruwe, alisema Mkuu huyo wa Wilaya.
Alisema agizo la kufunga shule hizo ambazo haliwagusi wanafunzi wa kidato cha kwanza na kidatu cha sita ambao alisema kutokana na umuhimu wao, wataendelea na masomo mpaka watakapofunga shule mwishoni mwa wiki hii.

Friday, 27 November 2009

VIMWANA WA WIKI


UDONGO WAOMBEWA UYAHUDI

MBUNGE wa Siha, Aggrey Mwanry, amechukua udongo wa Wilaya yake ya Hai na kuupeleka nchini Israel kwa ajili ya tambiko la kuombea wapiga kura wake waondokane na ukame na njaa.
Mwanry, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), alieleza hayo juzi kwenye mahafali ya darasa la saba katika Shule ya Punchimin iliyopo Kijiji cha Karansi, wilayani humo, mkoani Kilimanjaro.
Alisema jimbo lake limekuwa likikabiliwa na tatizo la ukame kwa muda mrefu linalosababisha wananchi kutaabika kwa uhaba wa chakula, hivyo amelazimika kuchukua udongo na kuupeleka nchini Israel alipozikwa Yesu, kwa kuwa ni nchi yenye ahadi na baraka.
“Mimi nimekuwa nikiumia sana pindi ninapoona wananchi wa jimbo langu mkitaabika na kuteseka kwa ajili ya tatizo la njaa. Watu wengi watajiuliza ni kwanini Mwanry ameamua kufanya hivyo, ila ni imani yangu kuwa tatizo hili litaisha tukimtegemea Mungu,” alisema.
Alisema kutokana na maombi hayo, tayari hali ya mvua inaimarika wilayani Siha, huku wananchi wakiwa na matarajio makubwa ya mazao katika msimu huu.
Alisema mpaka sasa wilaya hiyo tayari imekwishaanza kupandikiza mazao huku mengine yakionekana kuota katika sehemu mbalimbali za wilaya hiyo.
Hata hivyo, baadhi ya wadadisi wa masuala ya kisiasa na kiimani walisema hatua hii ya mbunge kutambika kwa udongo ni ya kishirikina.

MIKANDA YA ABIRIA KILA BASI

UKAGUZI na kamatakamata ya mabasi ambayo hayajafungwa mikanda katika viti vya abiria ilianza jana kwa mabasi yaendayo mikoani.Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Bw. James Kombe amesema shughuli hiyo imeanza baada ya kazi ya ufungaji mikanda kumalizika Novemba 26, mwezi huu.Alisema serikali ilitoa agizo hilo kwa wamiliki wa mabasi yaendayo mikoani na daladala kufunga mikanda hiyo katika viti kwa hiari lakini kwa sasa wakati huo umeisha na jeshi la kikosi cha usalama barabarani limesha sambazwa kuyakamata."Kwa sasa tumejipanga vizuri na tutahikisha tunakamata mabasi yote ambayo hayajafunga mikanda na kuyafikisha kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (SUMATRA) ili yatozwe faini kwa kukaidi kufunga mikanda hiyo kwa hiari," alisema Bw. Kombe.Alisema SUMATRA itakuwa inatoza faini kwa mabasi yasiyofunga mikanda kuanzia sh.200,000 na kuendelea ambapo shughuli hiyo inatarajiwa kuwa endelevu na baada ya kumaliza mabasi yaendayo mikoani watahamia kwa daladala.

Thursday, 26 November 2009

D'BANJ AWASILI BONGO

D'Banj amewasili nchini leo mchana kwa Ethiopian Airline kwa ajili ya shoo moja ya nguvu sana itakayofanyika siku ya jumamosi katika viwanja vya Tanganyika Packers ambapo yeye pamoja na wasanii kadhaa wa hapa nchini watafanya makamuzi ya kufa mtu siku hiyo.

LEO NI USIKU WA KINA BABA CLUBAFRIQUE




Wednesday, 25 November 2009

KIOTA CHA TEDDY BONGO


Tuesday, 24 November 2009

PASTA ALBINO...

Pasta kutoka nchini Canada Peter Ash ambaye pia ni mlemavu wa ngozi, akimpaka losheni mmoja wa wanafunzi ya shule ya Msingi Mitindo ambaye ni Albino alipotembelea shule hiyo katika wilaya ya Misungwi, mkoani Mwanza.
Picha na Patty Magubira

SPOTTED...

Songbird Whitney Houston with daughter Bobbi at the AMA.
Teairra Mari was spotted hanging out with rapper Hazel E this past weekend at Guys and Dolls in Hollywood.

Monday, 23 November 2009

SIKUKUU YA IDD EL HAJJ NI JUMAMOSI HII


Baraza Kuu la Waislamu Tanzania BAKWATA linawatangazia Wislamu na wananchi wote kwamba mwandamo wa mwezi Dhul Hajj umeonekana tarehe 18/11/2009 na kuashiria kuanza kwa mwezi mtukufu wa dhul Hajj (Mfungo Tatu)
Kwa maana hiyo sherehe ya sikukuu ya Eid el hajj itakuwa mwezi wa 10 dhul hajj sawa na Tarehe 28/11/2009 ( JUMAMOSI HII)


Sala na Baraza la Idd kitaifa zitafanyika katika msikiti wa Alfarouq uliopo Bakwata Makao Makuu Kinondoni Dar es alaaam , kuanzia saa 1.30 asubuhi na kufuatiwa na Baraza la Idd hadi saa 3.00 asubuhi.
Baraza kuu la Waislamu wa Tanzania BAKWATA linawatakia Eid njema waislamu wote na watanzania kwa ujumla


Imetolewa na Sheikh Ismail Habib
KAIMU MUFTI WA TANZANIA

POZI !!!

Toni Braxton na Mwanaye wa kiume
Amber Rose akiwa na Fabolous kwenye pati yake ya kuzaliwa jana usiku jijini New York.

RIHANNA...................

The chart-topper brought a distinctively hip air to the launch of the world's largest luxury liner, the Royal Caribbean's Oasis of the Seas in Florida.
Her choice of 'life-jacket orange' skin-tight dress and thigh-high black boots seemed to fit the bill
.

BUSTA RHYME AKAMUA VILIVYO BONGO

Busta Akigani misitari kwenye tamasha la FIESTA juzi ambapo aliacha mashabiki wake hoi jinsi alivyoshambulia jukwaa.
Hapa Busta katika pozi na wenyeji wake Bongo hoteli ya Kempiski kabla hajakwea pipa kwenda Marekani jana .Toka shoto ni Mrs Kusaga ,Teddy Mapunda , Busta na Joe Kusaga wakiwa na watoto wao.
Picha zaidi tembelea www.michuzijr.blogspot.com

Saturday, 21 November 2009

BUSTA RHYMES AWASILI KUKAMUA BONGO USIKU HUU

Mwanamuziki Busta Rymes kutoka nchini Marekani (katikati) akitoka kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu J.K.Nyerere mara baada ya kuwasili uwanjani hapo.Usiku huu anategemea kukamua FIESTA 2009 itakayofanyika katika viwanja vya posta kijitonyama.

Wednesday, 18 November 2009

RIPOTI YA IDADI YA WATU DUNIANI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dk Batilda Burian akizinduwa Ripoti ya Idadi ya watu Duniani Kulia Mwakilishi wa (UNFPA) Nchini Tanzania Dk Juliha Onabanjo katika ofisi za UN Kinondoni Dar es Salaam.

WANAUME KAMA MABINTI (VISERENGETI)

Kijana wa mjini, Mwilu Mwilola ‘Silvanus’ ambaye hivi karibuni alifumwa kitandani akiwa na Miss Mwanza 2006-07, Aunt Ezekiel kabla ya kutimuliwa na aliyekuwa mchumba wake, Sarah, anakuwa kipimo cha kwanza kwa sababu ‘ishu’ yake bado haijapoa.Silva, alifumwa akiwa na Aunt kitandani, wote wakiwa watupu kabla ya vurumai kuchukua nafasi, kwenye nyumba aliyokuwa anaishi, Kinondoni, jirani na Leaders Club, Dar es Salaam Alhamisi ya wiki iliyopita.Habari ya kufumaniwa iliandikwa kwa mara ya kwanza na gazeti hili, toleo lake la Jumamosi iliyopita kabla ya Ijumaa Wikienda kuandika ‘ishu’ ya Silva kutimuliwa na kuanza maisha upya, baada ya kunyang’anywa kila kitu na Sarah.Kwa ujumla, habari zilizothibitishwa na Sarah, ndugu pamoja na marafiki wa karibu, zinaeleza kuwa Silva alikuwa akilelewa na mchumba wake huyo wa zilipendwa na kuhudumiwa kwa kila kitu kabla ya kuachwa kwa aibu hapa ‘juzi-kati’.

‘Brazameni’ wa Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’, Charles Gabriel Mbwana ‘Chalz Baba’ naye yumo kwenye ‘listi’ baada ya hivi karibuni, mwanamke aliyekuwa akiishi naye, Mariam Ramadhan kumtimua kwa maelezo kuwa ni msaliti wa penzi lao.Mariam, alimtimua Chalz baada ya brazameni huyo kuangukia kwenye uhusiano wa kimapenzi na Miss Tanzania 2006-07, Wema Isaac Sepetu ‘The History’.Awali, Mariam alikuwa anaishi na Chalz Masaki, Dar es Salaam lakini baada ya kumtimua, hivi sasa mwana-Twanga huyo ‘anaminya’ kwenye ‘geto’ lake, Kinondoni Block 41, Dar.

Mwanamuziki mwingine wa Twanga, Kalala Hamza Junior hasahauliki kwenye orodha, yeye akitajwa kuishi ‘kisupastaa’ mjini kutokana na fedha za mrembo wake, Mary.Mbali na fedha, kwa sasa Kalala Jr hajui taksi wala daladala, badala yake ‘anaosha’ jina mjini kwa gari la Mary aina ya Toyota Nadia.

Twanga inaendelea kubeba ‘listi’ ya wanaume wanaopenda kulelewa kwa kumnyooshea kidole mwanamuzi ‘The Powerful Vocalist’, Saleh Kupaza ambaye kwa muda mrefu aliishi kwa nguvu ya mke wake, Mama Ife kabla ya kutengana.Saleh na Mama Ife, walitengana mapema mwaka huu baada ya mwanamuziki huyo kufumaniwa akiwa na mwanamke mwingine gesti.Mama Ife, ndiye aliyetinga kwenye ofisi za gazeti hili na kueleza kuwa yeye na Saleh basi, kabla ya kutangaza ndoa na aliyekuwa Meneja wa Televisheni ya C2C, Bahati Singh.Baada ya kuachana, Saleh alitunga wimbo unaopatikana kwenye albamu ya Mwana Dar es Salaam, unaoitwa Sitaki Kupenda ikiwa ni stori ya kweli, akielezea machungu aliyoyapata baada ya kupewa kisogo na Mama Ife.

Mwimbaji na rapa ‘The Amazing Vocalist’, Msafiri Said ‘Diouf’ ni mwanamuziki mwingine wa Twanga ambaye anadaiwa kuwa na hulka za kulelewa, akihusishwa na kimwana anayeitwa Mary, ingawa penzi lao haieleweki liliishia njia gani.

Dogo anayefanya kazi na Bendi ya FM Academia hivi sasa, Hassan Shaban ‘TX Moshi Jr.’ yupo kwenye namba ya wanaume wa hulka hiyo, yeye akidaiwa kuwekwa kinyumba na muigizaji Shumileta.Inaelezwa kwamba hivi sasa TX Jr. hataki tena kuishi kwenye nyumba yao ya Keko, badala yake ameamua ‘kuminya’ na Shumileta, Tabata, huku akitanua mjini na gari la muigizaji huyo.

Risasi Mchanganyiko linazo ‘data’ kuwa muigizaji ‘Mwili Jumba’, Gladys Chiduo ‘Zipompa’ aliwahi kumuweka kinyumba mwanamuziki wa zamani wa Bendi ya Diamond Sound, Zola Ndonga ambaye aliondoka kama alivyoingia pindi walipotibuana.

Kizito wa Kundi la Wateule, Jaffari Ally Mshamu ‘Jaffarai’ anaingia mzima mzima kwenye namba ya wanaume wanaolelewa kutokana na uhusiano wake wa kimapenzi na Meneja Uhusiano wa Benki ya NMB, Shyrose Bhanji.Kwa ujumla, penzi la Shyrose na Jaffarai siyo stori kutokana na kuandikwa mno na vyombo vya habari na inadaiwa kuwa nidhamu ya mwana-Hip Hop huyo ndiyo inayosaidia uhusiano wao kudumu mpaka leo.Katika uhusiano wao, Jaffarai amekuwa akipata huduma zote muhimu kutoka kwa Shyrose ambaye kutokana na kukolea kwa kijana huyo, huwa haoni ubahili ‘kukata pochi’ kumuwezesha ‘handsome boy’ wake.

Rais wa Bendi ya Akudo Impact, Christian Bella ‘Obama’ naye anatajwa kuwepo, akielezewa kwamba hivi sasa anapata matunzo yote kutoka kwa mwanamke anayefahamika kwa jina moja la Lillian.

Rapa wa FM Academia, Kitokololo a.k.a Kuku, pia anaongeza idadi ya wanaume wenye majina mjini ambao wanaishi kwa kulelewa na mademu zao, yeye akiwa amewekwa kinyumba na mwanamke aliyemzidi umri ‘jimama’, Sinza White Inn, Dar.Kabla ya kuhamia kwa mwanamke huyo, Kitokololo alikuwa anaishi na jimama lingine, Kinondoni, Dar kabla ya kutimuliwa kutokana na tabia yake ya ulevi wa kupitiliza kugeuka kero kwa mpenzi wake huyo.Risasi Mchanganyiko, hivi karibuni liliongea na Kitokololo ambaye alikiri kuhamia kwa jimama huyo, White Inn lakini akajigamba kwamba akiwa hapo, ni yeye ndiye ‘hukata pochi’ kwa ajili ya matumizi.

Mtangazaji wa Kituo cha Channel 10, Benny Kinyaiya anaingia moja kwa moja kwenye ‘listi’ kutokana na ile ‘ishu’ yake ya kutimuliwa na jimama na kutupiwa vyombo, ambayo iliandikwa magazetini.Katika sakata hilo, ilidaiwa kwamba Benny alikuwa akiishi kwa jimama hilo ambalo liliamua kumhudumia kwa kila kitu, lakini baadaye mwanamke huyo alimtimua kama vile hamjui baada ya penzi kutumbukia nyongo.

SOURCE : GPL

THE BOYZZ NDANI YA WANJA LETU LA NESHNO




KATUNI YA LEO


Tuesday, 17 November 2009

FIESTA ONE LOVE NDANI YA ZENJ (NGOME KUU)

Wazee wa samaki hao ni balaa moto wa kuotea mbali uliza wazenj watakupa habari zao.
Alikiba kama kawaida akilishambulia jukwaa sijui lini atakuja Ukerewe mapromota changamkeni basi jamaa anasubiliwa kwa hamu.

Sehemu ya umati uliokuwepo ngome kuu.


Monday, 16 November 2009

SHEREHE ZA UHURU WA TANZANIA UKEREWE

5th DEC 2009 TANZANIA INDEPENDENCE CELEBRATION IN LONDON
BONGODJS PROUDLY PRESENTS CELEBRATION OF TANZANIA INDEPENDENCE DAY ON SAT 5TH DECEMBER 2009 @ THE PRESTIGEOUS LA ROYALE BANQUENTING SUITES 819-821 HIGH ROAD TOTTENHAM LONDON N17 8ER FROM 7PM-3AM FOR ONLY£15 COME AND ENJOY LIVE BAND BONGODJS ON THE MIX,PS PASS THE MESSAGE AROUND!SPECIAL NITE NOT TO BE MISSED!!!

SPONSORED BY
SWIFT FREIGHTS UK
TZUK.com & BONGOTIMES

RAISI JK NA "MO FOUNDATION" NDANI YA MLIMANI CITY

JK akiteta na Yossou N'dour na Lady Jaydee
Hapa Rais akiwachekesha Bw. na Bi. Habash baada ya JD kuangusha shoo la nguvu na vijana wa nyumba ya vipaji (THT).

Saturday, 14 November 2009

NOLLYWOOD ACTOR KIDNAPPED

Actor Nkem Owoh has been kidnapped.
Mr. Owoh is one of the top Nollywood actors mainly due to his role in the blockbuster movie ‘Osuofia in London ’. He was kidnapped along the Enugu – PortHarcourt Expressway Nigeria and his kidnappers have reportedly demanded a 15 million naira ransom.

'worst storm of the year' causes Chaos

Gale-force winds and heavy rain brought flooding and damage to Britain today as parts of the country were battered by gusts of up to 100mph.
The lighthouse at The Needles on the westernmost point of the Isle of Wight reported gusts of between 95mph and 100mph.
In West Sussex, fire crews were called to two lightning strikes, and motorists had to be rescued from cars in Dorset after getting caught in flash floods.
The Environment Agency has 24 flood warnings in force, with the majority in southern coastal regions.
Stephen Davenport, of MeteoGroup UK, said: 'This is the strongest storm we have had this year, but it is just an autumnal storm, and not untypical for this time of year

RISASI JUMAMOSI


HARUSI YA VERO NA MATHEW LEO


Wakitoka kanisani St.Joseph mara baada ya kufunga ndoa yao.Kwa picha zaidi bofya hapa www.michuzijr.blogspot.com

Friday, 13 November 2009

MAMA KIKWETE KWENYE SHOO YA UTEPE MWEUPE



Mke wa Rais mama Salma Kikwete ambaye pia ni mwenyekiti wa Taasisi ya wanawake na Maendeleo (WAMA) akimweleza jambo Balozi wa kimataifa wa Utepe na msanii na mwanamitindo wakati wa onyesho la mavazi lililoandaliwa na Taassi ya Utepe Mweupe.
Na Anna Nkinda – MAELEZOJumla ya dola za kimarekani 10,000/= zimepatikana kutokana na mnada wa nguo ya kike iliyotolewa na msanii na mwanamitindo wa Kimataifa Naomi Campbell katika maonesho ya mavazi ya Relief Tanzania yaliyofanyika jana usiku katika ukumbi wa Movenpick jijjini Dar es Salaam.Maonesho hayo yaliandaliwa na Naomi Campbell ambaye ni Balozi wa Kimataifa wa Utepe Mweupe kwa kushirikiana na Mustafa Hassanali ambaye ni mwanamitindo wa hapa nchini kwa lengo la kukusanya fedha ili kutunisha mfuko wa Mtandao wa Utepe Mweupe (The White Ribbon Alliance).Akiongea mara baada ya maonesho hayo Campbell alisema lengo la kufanya maonyesho hayo ni kupata fedha ambazo zitatumika katika kampeni ya kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto.Kuhusu wabunifu wa mavazi na wanamitindo wa hapa Tanzania alisema anaridhishwa na kazi zao na wanajitahidi kufanya kazi nzuri kwa ufasaha mkubwa na kwa kujituma.Aliendelea kusema kuwa anaipenda nchi ya Tanzania kwa sasabu inavivutio vingi kama vile mbuga za wanyama, visiwa vya Zanzibar, mito, milima, maziwa na Bahari ya Hindi huku akisisitiza kuwa si mara ya kwanza kuja Tanzania na ana wa kuendelelea kuja hapa nchini.Katika maonyesho hayo Mke wa Rais Mama Salma Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) pamoja na Mke wa Rais wa Zambia Mama Thandiwe Banda walihudhuria.Mtandao wa Utepe Mweupe (White Ribbon Alliance) wenye takribani nchi wanachama 143 duniani ambao jana uliadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa kwake unafanya kazi kubwa yakuhakikisha kuwa nchi wanachama zinaondokana na vifo vya kina mama wajawazito wakati wa kujifungua.

APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO IKULU

Rais Jakaya Kikwete akipokea hati za utambulisho kutoka kwa balozi mteule wa nchi ya Rwanda mheshimiwa Fatuma Ndangiza Nyirakobwa .

SIMANZI WILAYANI SAME

SIMANZI na vilio jana vilitawala kwenye mazishi ya watu 2O waliofariki dunia kwa kufunikwa na kifusi kilichoporomoka mlimani na kufukia nyumba zao usiku wa manane katika Kata ya Mamba Miamba, wilayani Same, Kilimajaro.
watu zaidi ya 1,000 waliokusanyika katika msiba huo mkubwa wakiwa wamefunikwa na simazi, huku wakilia kwa uchungu kutokana na kupoteza ndugu zao katika mkasa huo wa kutisha.
Asilimia kubwa ya watu walionyesha masikitiko yao, hasa kwa familia ambayo imepoteza watu 15 na kati ya hao wanne hawajapatikana mpaka sasa.
Wanachi hao waliiomba serikali iwasaidie kutafuta miili ya watu hao na ikiwezekana watumie kikosi cha mbwa ili kubaini mahali ilipo.
Elineema Shambi, mmoja wa ndugu wa wanafamilia 15 waliofariki dunia na ambaye alinusurika kwa vile alikuwa amekwenda mjini Moshi kwa shughuli za kibiashara, alisema kwa majonzi kwamba amepoteza mke na watoto wake wanne ambao walifukiwa na kifusi hicho.
Alisema alikwenda mjini Moshi kununua bidhaa za kuuza, na kesho yake asubuhi alipigiwa simu na kuondoka mara moja. Alieleza kuwa alipofika alikuta nyumba yake imefunikwa kabisa kiasi cha kutoonyesha kama kulikuwa na nyumba na mwili wa mkewe ulikuwa haujapatikana hivyo akasaidia kuutafuta na kuupata pamoja na miili ya watoto wake.
Alifahamisha kuwa yeye ni mmoja kati ya ndugu wa watu 15 waliofariki katika tukio hilo la kutisha.
Akisimulia juu ya maporomoko hayo, alisema, dalili za mlima huo kuporomoka zilianza kuoneka mwaka jana kwa kuwa kulikuwa na ufa, hata hivyo hakueleza kwamba ni kwa nini hawakuhama katika eneo.
Akiunga mkono maelezo hayo, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Monica Mbega alibainisha kuwa wananchi wa Kata ya Mamba Miamba walishaona dalili za kuporomoka kwa mlima ulioua watu 20, tangu mwaka jana, lakini hawakuchukua tahadhari.
Wakati Mbega akisema hayo, Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) imesema haikuweza kutoa taarifa ya kutahadharisha wananchi dhidi ya janga hilo kwa kuwa vipimo vyake havikuweza kutabiri mvua kubwa.
Mbega alitoa kauli hiyo jana katika eneo hilo la maafa wakati akiongoza maelfu kwa mamia ya wananchi wa eneo hilo na kutoka nje ya Wilaya ya Same katika mazishi ya watu waliofariki kutokana na janga hilo.
Mkuu huyo wa mkoa alisema uchunguzi wa awali umebaini kuwa mlima huo ulianza kuonyesha ufa mwaka jana na baadaye Mei mwaka huu ufa huo ukazibika, lakini kumbe ndani ya mlima bado ulikuwa umeacha shimo kubwa.
Kwa mujibu wa Mbega, ambaye pia ni mbunge wa Iringa Mjini, pamoja na dalili zote hizo wananchi hao hawakuchukua hatua za tahadhari ikiwamo kutoa taarifa kwa mamlaka zinazohusika ikiwamo serikali.
RC Mbega alisema endapo wananchi wangetoa taarifa mapema, serikali ingeweza kutuma wataalamu wake ambao wangesaidia kushauri jinsi ya kuepuka janga hilo.
Hadi kufikia jana saa 9:00 alasiri, miili ya watu wazima 19 na mtoto mchanga wa miezi tisa ilikuwa imeopolewa kutoka katika vifusi vilivyoporomoka kwenye mlima huo wenye majabali makubwa ya mawe.
Madaktari walilazimika kufanya upasuaji kwenye maiti ya mwanamke aliyejulikana kama Wemael Mhina, 30, ambaye ingawa siku zake za kujifungua zilikuwa zimeshatimia, hakujifungua hadi alipofikwa na mauti hayo.
Mkuu wa mkoa alisema Rais Jakaya Kikwete, Waziri wa Kilimo,Chakula na Ushirika, Steven Wassira na Naibu Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia, Maua Daftari wametuma salamu za rambirambi.
Katika kuungana na wafiwa katika msiba huo mkubwa, Mbega alisema serikali imetoa Sh2 milioni za rambirambi kwa wafiwa na kugharamia shughuli zote za mazishi, ikiwa ni pamoja na chakula, malazi, matibabu na majeneza.
Mkuu wa Wilaya ya Same, Ibrahim Marwa ameiomba serikali kutuma wataalamu wa miamba katika maeneo ya wilaya hiyo ili kuchunguza uhimili wake hasa kutokana na mvua nyingi zinazoendelea.
Marwa alisema tukio la kuporomoka kwa mlima liliwahi kutokea katika eneo la Hedaru, lakini halikusababisha madhara hivyo akasema upo umuhimu wa uchunguzi kufanyika.
Pia mkuu huyo wa wilaya aliuomba uongozi wa serikali na Jeshi la Polisi kutuma kikosi chake cha mbwa ili kusaidia kazi ya kutafuta miili ya watu wanne ambao wanaaminika bado wamenasa chini ya kifusi cha tope.
Marwa alisema mbwa hao watakuwa msaada mkubwa wa kubaini sehemu ambazo watakuwa wamefukiwa watu hao kutokana na mbwa hao kuwa na utaalamu na ujuzi wa kubaini mambo ya namna hiyo kwa kunusa.
Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Dk Mathayo David ambaye pia ni mbunge wa Same Magharibi, alisema msiba huo ni mkubwa na kwamba umemgusa.
Viongozi wengine waliohudhuria mazishi hayo ni pamoja na wakuu wa wilaya zote za mkoa wa Kilimanjaro isipokuwa Wilaya ya Siha, wakurugenzi wa halmashauri za wilaya jirani,viongozi wa dini na wananchi.
Wakati wa mazishi hayo, kitongoji hicho cha Manja kilizizima kwa vilio na kwikwi kutokana na ukweli kuwa wengi waliofariki ni ndugu wa familia moja huku familia moja ikipoteza baba, mama na watoto wanne.
Eneo moja la makaburi kumezikwa ndugu tisa wa familia ambao walipoteza maisha katika tukio, wakati eneo jingine wamezikwa ndugu tisa wa familia moja huku eneo jingine wakizikwa ndugu wanne wa familia moja.
Shughuli za mazishi hayo zilianza saa 8:00 mchana na saa 9:15 alasiri ndipo waombolezaji walipoanza kazi rasmi ya kuzika huku simanzi kubwa ikionekana dhahiri miongoni mwa waombolezaji.
Wakati huohuo, Makoba Hassan na Thomas Ludovick wanaripoti kuwa TMA imesema haikuweza kuitahadharisha jamii kuhusu maafa yaliyotokea wilayani Same mkoani Kilimanjaro kwa sababu ya mvua kwa kuwa vipimo vyake havikuweza kutabiri.
Kaimu Mkurugenzi wa shughuli za utabiri nchini, Matitu Mohammed alisema jana ofisini kwake kuwa hali hiyo ilitokea kutokana na vipimo vyao vya utabiri wa hali ya hewa wilayani hapo kuwa mbali na eneo lililotokea tukio hilo.
"Tukio lilitokea sehemu za milimani ambako vipimo vyetu vya utabiri vilishindwa kurekodi na kutoa taarifa kwa watu wa eneo hili kutokana na kituo chetu kuwa mbali," alisema Mohammed.
Alisema dhana kuwa mvua hizo ni El-Nino si ya kweli bali mvua hizo kitaalamu zinaitwa mvua za vuli ambazo hutokea katika kipindi hiki na husababishwa na ongezeko la joto katika Bahari ya Pacific
"Naomba wananchi waelewe kuwa hakuna mvua za El-Nino bali ni mvua za vuli ambazo huambatana na mfumo wa pepo zinazovuma kutoka Bahari ya Pacific kuelekea Bahari ya Hindi hivyo kusababisha mvua kubwa kutokea katika maeneo yote duniani," alisema.
Alizitaja sehemu zilizowahi kutokea maafa katika kipindi kilichopita kuwa ni Hedaru, Makanya, katikati ya Same na Mwanga na Same yenyewe kwa sasa ikiwa ni mara ya pili.

MISS UNIVERSE TANZANIA 2009


Miss Universe Tanzania Iluminata James katika pozi uwanja wa kimataifa wa Ml Julius Nyerere jijini DSM kabla hajakwea pipa kuelekea Chengdu ,Nchini Uchina ambako yatafanyika mashindano ya mwaka huu.

Monday, 9 November 2009

LADYZZZZZZZZZ...

Singer Frenchie Davis and actress Kim Coles attended the 12th Annual GLAAD Tidings Season’s Greenings with Kim in a figure flattering all black outfit punctuated by a sequin tank, and Frenchie in a peachy pink wrap dress and gold sandals. Kim looks hot and sophisticated in her chic outfit and bow front sandals, but hmm, Frenchie…I don’t think the peak-a-boo lace bra works here. She certainly look saucy, but perhaps this dress would have benefited from either a lower cut bra or a cute comfy camisole.

KIPANYA ......................







UMEME WA IPTL WAINGIZWA KWENYE GRIDI YA TAIFA

HATIMAYE mtambo mmoja kati ya mitambo 10 ya Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), umewashwa na kuanza kuingiza mewagati za umeme 10 katika gridi ya Taifa.Akizungumza Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo, Dk. Magesvaran Subramanian, alikiri kuwashwa kwa mtambo huo na kuongeza kuwa uliwashwa rasmi jana saa 6.04 mchana.“Tumeanza kufanya kazi na mtambo mmoja namba moja ndio uliowashwa na mpaka sasa kila kitu kinakwenda vizuri tunatarajia mpaka kesho (leo), utakuwa umeshaanza kuzalisha megwati zote kumi,” alisema Dk. Subramanian.Naye Mfilisi wa kampuni hiyo, Rugonzibwa Mujunangoma, alisema mtambo huo uliwashwa jana, lakini kwa wakati ule haukuweza kuzalisha umeme wote wa megawati 10 na kwamba kadri ulivyokuwa ukiendelea kuzalisha umeme, ndipo megawati zilipokuwa zikiendelea kupanda na kufika 10.“Tangu mtambo uwashwe na hadi ninaondoka muda wa saa saba mchana, mtambo tayari ulishaanza kuingiza megawati 1.5, lakini hadi kesho (leo)), utakuwa tayari unazalisha megawati kumi, ikumbukwe hii ni mashine,” alisema Rugonzibwa.Kuhusu mitambo mingine tisa, alisema mafundi na watalaamu wa masuala ya umeme wanaendelea na ukaguzi ambapo nayo haitochukua muda mrefu itawashwa wakati wowote.“Kuwaka kwa mtambo huu ni dalili nzuri kuwa mitambo mingine nayo haitochukua muda itawaka, mafundi wanaendelea vizuri na kazi yao na kwa kweli hali inatia matumaini,” alisema mfilisi huyo.Kampuni hiyo ya IPTL ina mitambo 10 ambayo kila mmoja ukiwaka utatoa megawati 10 na hivyo mtambo mzima wa IPTL unatarajiwa kutoa megwati 100, na hivyo kupunguza tatizo la mgawo wa umeme ambalo limeikumba nchi kutokana na kuharibika kwa mitambo ya Kihansi na Songas.Rais Jakaya Kikwete aliagiza katikati ya mwezi uliopita kwa mamlaka husika kuwa mitambo hiyo ya IPTL iwashwe ifikapo Novemba mosi, mwaka huu ili kukabiliana na tatizo la mgawo. Imechelewa kuwashwa kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kuchelewa kwa malipo kwa taasisi zitakazohusika kuendesha mitambo hiyo.

Sunday, 8 November 2009

USIKU WA MAGITAA CLUBAFRIQUE

LEO USIKU WA JUMAPILI VIJANA WA "SOUND AFRIQUE BAND" KAMA KAWAIDA WATABURUDISHA KUANZIA SAA 4 USIKU HADI SAA TISA MAJOGOO KATIKA UWANJA WAO WA NYUMBANI 147 BARKING ROAD,CANNING TOWN, LONDON E16 4HQ

MOTO WATEKETEZA "MAISHA CLUB" OYSTERBAY

Kiota cha kujiachia cha Maisha Club kilichopo Oysterbay jijini Dsm leo mchana kimeteketea kwa moto, taarifa zilizopatikana kutoka kwa mashuhuda wamesema kuwa kulikuwapo na ukarabati uliokuwa unaendelea wa vipupwe (AC),kwa bahati mbaya wakati wa ukarabati huo mojawapo ikalipuka kutokana na nyaya zake kugusana,na baadaye moto mkubwa ukazuka katika jengo hilo,imeelezwa kuwa taarifa zilifika kwa watu wa zima moto lakini hawakuwahi kuuzima moto huo kwa haraka kwani kwa asilimia kubwa vitu vilivyokuwemo vilikuwa vimekwishateketea.

Saturday, 7 November 2009

MAZISHI YA MZEE ALEX KUSAGA KATIKA PICHA