SHEREHE za Yanga kutwaa taji la 24 la ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara zimefana jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Hiyo inafuatia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya watani wao jadi Simba SC katika mchezo wa kufunga pazia la ligi hiyo.
Kwa matokeo hayo, Yanga inamaliza msimu wa Ligi Kuu ikiwa na pointi 60, ikifuatiwa na Azam FC yenye 52 na Simba 45
Katika mchezo huo, uliochezeshwa na refa Martin Saanya wa Morogoro, aliyesaidiwa na Samuel Mpenzu wa Arusha na Jesse Erasmo kutoka Morogoro, hadi mapumziko Yanga walikuwa mbele kwa bao 1-0 lililotiwa kimiani na Didier Kavumbangu dakika ya tano tu.
Kavumbangu alifunga kwa kichwa akiuwahi mpira wa juu uliopanguliwa na kipa na Nahodha wa Simba, Juma Kaseja kufuatia kona iliyochongwa na Haruna Niyonzima kutoka wingi ya kushoto. Mpira uliozaa kona hiyo ulitokana na Simon Msuva ambaye alikuwa anachanja mbuga, lakini beki Haruna Shamte akatoa nje.
Simba ilipata nafasi ya kusawazisha dakika ya 27 baada ya Mrisho Ngassa kuangushwa kwenye eneo la hatari na Nadir Cannavaro na refa Saanya kuamuru penalti, lakini mkwaju wa Mussa Mudde ulipanguliwa na Ally Mustafa ‘Barthez’ kabla ya kipa huyo kuuchupia na kuudaka.
Kwa ujumla, Yanga ilitawala kipindi ca kwanza karibu chote ingawa mwishoni mwa kipindi hicho, kidogo Haruna Chanongo aliitia majaribioni ngome ya Yanga kama mara mbili hivi na kusababisha kona mbili mfululizo.
Kipindi cha pili, Simba SC walikianza vizuri dakika 10 za mwanzo wakipeleka mashambulizi langoni mwa Yanga kutokea pembeni, lakini safu ya ulinzi ya mabingwa hao wa Bara ilisimama imara kukabiliana na hatari zote.
Krosi maridadi ya Simon Msuva dakika ya 62 iliunganishwa vyema kimiani na Hamisi Kiiza ‘Diego’ kuipatia Yanga bao la pili. Baada ya bao hilo, Yanga sasa walianza kucheza kwa kujiamini zaidi na Simba wakionekana kucheza ili kutoruhusu mabao zaidi.
Dakika 87 ya refa alijeruhiwa wakati anakwenda kuamua ugomvi kati ya Didier Kavumbangu na Nassor Masoud ‘Chollo’ akaanguka na kutibiwa kwa dakika hadi kuinuka dakika ya 90 na kumaliza mpira baada ya sekunde kadhaa.
Simba SC - Juma Kaseja, Nassor Masoud ‘Chollo’, Haruna Shamte, Mussa Mudde, Shomary Kapombe, William Lucian ‘Gallas’, Mrisho Ngassa, Mwinyi Kazimoto, Abdallah Seseme/Ranmadhani Singano ‘Messi’, Amri Kiemba/Jonas Mkude na Haruna Chanongo/Felix Sunzu.
Yanga SC - Ally Mustafa ‘Barthez’, Mbuyu Twite/Juma Abdul, David Luhende, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Frank Domayo, Didier Kavumbangu na Hamisi Kiiza/Niaar Khalfan.
KWA HISANI YA BIN ZUBEIRY
Saturday, May 18, 2013
Friday, May 17, 2013
HUDUMA MPYA YA USAFIRI WA RELI JIJINI DSM IKO NJIANI
Mh. Dk. Harrison Mwakyembe amesema wizara ya Uchukuzi inaangalia uwezekano wa kuanzisha huduma maalumu ya kati ya Stesheni ya Dar es Salaam na Gongo la Mboto kwa ajili ya kuhudumia abiria wanaoshukia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Dk Mwakyembe alisema hivi sasa wanatafuta mchakato wa kumpata mwekezaji na mwendeshaji wa huduma ya usafiri wa treni ya abiria katika jiji la Dar es Salaam.
“Mwekezaji huyo atatumia miundombinu ya reli iliyopo, vichwa vya treni na mabehewa maalumu kwa ajili ya usafiri wa abiria katika Jiji,” alisema Dk Mwakyembe, ambaye Wizara yake imeomba Sh491,105,994,000 katika bajeti hiyo, Sh100,584,174 zikiwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida na Sh390,521,220,00 kwa shughuli za maendeleo.
Alisema usafiri wa reli Dar es Salaam umesaidia kupunguza idadi ya magari barabarani kwani abiria 14,000 wanaotumia reli hiyo kwa siku wangehitaji mabasi 467.
Alisema wizara yake imetenga Sh113.1 bilioni kwa ajili ya kukamilisha ununuzi wa vichwa vinane vya treni, mabehewa 22 ya abiria, mabehewa 274 ya mizigo na mabehewa 34 ya breki.
Wednesday, May 15, 2013
KUTOKA UBALOZINI HAPA UK ...............

MAAFISA WA UBALOZI WETU HAPA UINGEREZA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA MH. CHABAKA KILUMANGA ( ALIYESHIKA MAUA)ALIYEKUA NAIBU BALOZI HAPA UK AMBAYE HIVI KARIBUNI AMECHAGULIWA NA MHESHIMIWA RAISI KUWA BALOZI WETU COMORO
Tuesday, May 14, 2013
REDD MISS IFM WAKO TAYARI
Warembo wa Redd’s Miss IFM wakiwa katika picha ya pamoja.
Meneja wa Kinywaji cha Redd's Victoria Kimaro katikati akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es salaam juu ya maandalizi ya shindano la Redd's Miss IFM 2013.
Mratibu wa Redd’s Miss IFM, Daniel Sarungi katika akizungumza na waandishi wa Habari jijini dar es salaam juu ya shindano la Redd's IFM linalotarajiwa kufanyika May 25,2013, kulia ni meneja wa Kinywaji cha Redd's Victoria Kimaro
PICHA YA LEO

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais mstaafu wa Nigeria na Balozi wa heshima wa IITA Chief Olesegun Obasanjo na Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee Benjamin William Mkapa katika picha ya pamoja na wadau wa maendeleo bnaada ya kuzindua rasmi jengo la sayansi katika kituo cha Taasisi ya Kimataiafa ya Kilimo cha Tropiki (IITA) Mikocheni jijini Dar es salaam leo Mei 13, 2013.Picha na IKULU
Monday, May 13, 2013
UZINDUZI WA MSIMU MPYA WA CLOUDS FM DODOMA WAFUNIKA

Msanii wa muziki wa kizazi kipya ajulikanae kwa jina la Snura akiimba jukwaani wimbo wake unaotamba kwa sasa katika vituo vingi vya redio,uitwao Majanga,mbele ya maelfu ya watu waliofika kwenye uwanja wa Jamuhuiri jioni ya leo wakati wa kituo cha redio ya Clouds FM ilipokuwa ikizindua msimu wake mpya kwa wasikilizaji wake,uzinduzi huo ulikwenda sambamba na kufanyika kwa semina ya fursa kwa Watanzania.
Msanii mahiri wa Mashairi hapa nchini,Mrisho Mpoto akiwakuna vilivyo wakazi wa mji wa Dodoma alipowaangushia maneno kadhaa na umati kulipukwa na mayowe kila kona,ambapo Clouds FM wamezindua msimu wao mpya.
Maelfu ya Watu wakiwa ndani ya uwanja wa jamhuri wakijumuika kwa pamoja na wana Clouds FM walipokuwa wakizindua msimu wao mpya.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya a.k.a bongofleva katika miondoko ya Hip Hop,Izzo Bizziness akikamua kwa shangwe kubwa mbele ya maelfu ya wakazi wa mji wa Dodoma waliofika ndani ya uwanja wa Jamuhuri,walipokwenda kushuhudia uzinduzi wa msimu mpya wa Clouds FM.
Mkurugenzi wa vipindi na Utafiti,Ruge Mutahaba akizungumza na Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye ndani ya Uwanja wa Jamuhuri jioni ya leo,wakati tamasha la uzinduzi wa msimu mpya wa Clouds FM likiendelea,Nape alifika uwanjani hapo kujionea shamrashamra mbalimbali zilizojumuisha maelfu ya watu.
Palikuwa hapatoshi uwanja wa jamhuri Dodoma .
Picha na Habari kwa hisani ya SHAFFI DAUDA
MH. RAIS DKT JAKAYA KIKWETE ATEUA MABALOZI WAPYA

Rais Jakaya Kikwete

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, amefanya uteuzi wa Mabalozi Wapya kujaza nafasi zilizo wazi na kuanzisha Ofisi za Ubalozi nchini Uholanzi na Comoro. Aidha Mheshimiwa Rais amefanya uhamisho wa Balozi kutoka kwenye kituo kimoja.
Mabalozi wateule na aliyehamishwa kituo ni kama ifuatavyo:-
Bw. Wilson M. K. Masilingi;
Ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi. Bw. Masilingi ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kituo cha Mikutano cha Kimataifa, Arusha, (AICC) na aliwahi kuwa Mbunge katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kati ya mwaka 1995 – 2010. Aidha, katika kipindi cha mwaka 1998 – 2005 alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais mwenye dhamana ya masuala ya Utawala Bora.
Bw. Chabaka Faraji Ali Kilumanga, ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Comoro. Hadi uteuzi huu unafanyika, Bw. Kilumanga alikuwa Balozi Mdogo katika ofisi ya Ubalozi nchini Uingereza.
Bw. Modest Jonathan Mero, ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania kwenye Ofisi za Umoja wa Mataifa, Geneva. Kabla ya uteuzi Bw. Mero alikuwa Afisa wa Mambo ya Nje Mwandamizi kwenye Ubalozi wa Tanzania katika Ofisi za Umoja wa Mataifa, New York.
Kadhalika, Mheshimiwa Rais amemhamisha Balozi Philip Sang’ka Marmo kutoka Ubalozi wa Jamhuri ya Watu wa China na kwenda Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani.
Mabalozi wateule na aliyehamishwa kituo ni kama ifuatavyo:-
Bw. Wilson M. K. Masilingi;
Ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi. Bw. Masilingi ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kituo cha Mikutano cha Kimataifa, Arusha, (AICC) na aliwahi kuwa Mbunge katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kati ya mwaka 1995 – 2010. Aidha, katika kipindi cha mwaka 1998 – 2005 alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais mwenye dhamana ya masuala ya Utawala Bora.
Bw. Chabaka Faraji Ali Kilumanga, ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Comoro. Hadi uteuzi huu unafanyika, Bw. Kilumanga alikuwa Balozi Mdogo katika ofisi ya Ubalozi nchini Uingereza.
Bw. Modest Jonathan Mero, ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania kwenye Ofisi za Umoja wa Mataifa, Geneva. Kabla ya uteuzi Bw. Mero alikuwa Afisa wa Mambo ya Nje Mwandamizi kwenye Ubalozi wa Tanzania katika Ofisi za Umoja wa Mataifa, New York.
Kadhalika, Mheshimiwa Rais amemhamisha Balozi Philip Sang’ka Marmo kutoka Ubalozi wa Jamhuri ya Watu wa China na kwenda Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani.
------MWISH0-----
(John M. Haule)
KATIBU MKUU,
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA,
DAR ES SALAAM.
12 MEI, 2013
Saturday, May 11, 2013
MAZISHI YA WALIOFARIKI KWENYE MLIPUKO KANISA KATOLIKI ARUSHA
Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, Freeman Mbowe
akiweka shada la maua katika moja ya makaburi hayo. (PICHA NA SEIF MANGWANGI)
baadhi ya majeneza yenye miili ya marehemu ikiwa kanisani tayari kuombewa
Thursday, May 09, 2013
LONDON IS THE WORLD MILLIONAIRES PLAYGROUND
While global financial meltdown and double-dip recessions have left many of us counting the pennies, it seems that the streets of London are still paved with gold for some.
The UK capital is home to more multimillionaires than any other city in the world according to new figures.
London boasts a staggering 4,224 'ultra-high net worth' residents - people with a net worth of more than $30million, or £19.2million.

Millionaires playground: London boasts the highest number of individuals worth more than £19million in the world

Super-rich: Areas such as Knightsbridge, picture, Mayfair and Kensington, where property prices are particularly expensive, are home to many of London's super-rich

Wealthy: London is now home to a staggering 4,224 multi-millionaires
Wednesday, May 08, 2013
JAGUAR - KENYAN ARTIST FORTUNES

Take a look at his fortunes;
1. Owns a fleet of cabs called “Jagz Cabs”
2. Possesses a motor garage in industrial area
3. Four cars worth KShs.20M.
4. Contracts with key corporates like EABL, Safaricom and Unilever which earns him upto
KShs.18M for a half-year contract deal. This would mean that Jaguar’s contracts alone can get him up to KES 3 million a month for six consecutive months.
5. KShs.15M home
6. Music performances where he gets about KShs.300,000 per appearance
7. Matatu fleet plying several routes in Nairobi.
8. Owns the Response Security Co. Ltd.
Tuesday, May 07, 2013
MAUA SAMA MOTO UWAKAO KASI KATIKA KIZAZI KIPYA
Maua Sama ni msanii chipukizi kutoka Moshi. Ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo Cha Ushirika na Biashara Moshi.
Maua ni almasi mchangani ambayo imegunduliwa na MwanaFA baada ya kupata ‘demo’ yake aliyofanyia studio za Moshi na kuipeleka mbele ya “Management Team” yake Lifeline/T.I.A ambao moja kwa moja wakamchukua. Maua anafanya kazi chini ya uangalizi wa Lifeline/T.I.A Inc; Label ya muziki ambayo inasimamia kazi za muziki za MwanaFA. So Crazy ambao ni wake wa kwanza umetayarishwa na producer Marco Chali wa MJ Records na amemshirikisha MwanaFA. Mipango iliyopo ni kumfanya Maua Sama kuwa mwimbaji bora wa muziki Tanzania.
BOFYA HAPO CHINI UMSIKIE.
FBI WATUA ARUSHA
Wakati maofisa wa Shirika la Upelelezi wa Marekani (FBI) wametua Arusha, raia wanne wa Saudi Arabia na Watanzania wawili wamekamatwa kwa tuhuma za kuhusika kulipua bomu lililoua watu wawili na kujeruhi wengine 61 wakati wa ufunguzi wa Kanisa la Mtakatifu Joseph Parokia ya Olasiti.
Waliofariki dunia ni Regina Longino Kurusei (45), mkazi wa Olasiti na James Gabriel (16), ambaye alifariki usiku wa kuamkia jana.
Tukio hilo lilitokea wakati Balozi wa Vatican na Mwakilishi wa Papa nchini, Francisco Montecillo Padilla alipokuwa akizindua kanisa hilo.
Akitoa maelezo kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda jana, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo alisema raia hao wa Saudi Arabia walikamatwa jana asubuhi baada ya tukio wakiwa kwenye gari wakielekea Kenya kupitia Namanga.
Mulongo alisema raia hao wa kigeni waliingia nchini Jumamosi iliyopita na siku iliyofuata ndipo kukatokea ulipuaji huo. Alisema lengo la shambulizi hilo lilikuwa kumdhuru Askofu Padilla.
“Mtu ambaye tulimkamata jana (juzi Jumapili) ndiye aliyesaidia kuwapata watu hawa wa Saudi Arabia na Watanzania hao,” alisema Mulongo.
Mulongo alisema maofisa wa FBI walifika jana saa tano asubuhi ili kusaidiana na Polisi na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), katika uchunguzi wa tukio hilo.
Maofisa hao wa FBI walikuwa Zanzibar ambako walikuwa wanachunguza kifo cha Padri Evaristus Mushi ambaye aliuawa Februari 17, mwaka huu.
Waliofariki dunia ni Regina Longino Kurusei (45), mkazi wa Olasiti na James Gabriel (16), ambaye alifariki usiku wa kuamkia jana.
Tukio hilo lilitokea wakati Balozi wa Vatican na Mwakilishi wa Papa nchini, Francisco Montecillo Padilla alipokuwa akizindua kanisa hilo.
Akitoa maelezo kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda jana, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo alisema raia hao wa Saudi Arabia walikamatwa jana asubuhi baada ya tukio wakiwa kwenye gari wakielekea Kenya kupitia Namanga.
Mulongo alisema raia hao wa kigeni waliingia nchini Jumamosi iliyopita na siku iliyofuata ndipo kukatokea ulipuaji huo. Alisema lengo la shambulizi hilo lilikuwa kumdhuru Askofu Padilla.
“Mtu ambaye tulimkamata jana (juzi Jumapili) ndiye aliyesaidia kuwapata watu hawa wa Saudi Arabia na Watanzania hao,” alisema Mulongo.
Mulongo alisema maofisa wa FBI walifika jana saa tano asubuhi ili kusaidiana na Polisi na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), katika uchunguzi wa tukio hilo.
Maofisa hao wa FBI walikuwa Zanzibar ambako walikuwa wanachunguza kifo cha Padri Evaristus Mushi ambaye aliuawa Februari 17, mwaka huu.
Monday, May 06, 2013
Sunday, May 05, 2013
KANISA LA RC ARUSHA LASHAMBULIWA NA WAUMINI WENGI WAJERUHIWA
BREAKING NEWS ............
Leo kulikuwa na uzinduzi wa Parokia mpya ya Olasit mjini Arusha. Mgeni rasmi alikuwa Mwakilishi wa Papa toka Vatican. Kulikuwa na wageni wengi waliambatana na mwakilishi wa papa, wakiwemo maaskofu, mapadre na watawa kutoka mataifa mbalimbali.
Mtoto mmoja ameeleza kuwa aliona watu waliokuwa kwenye mini bus wakirusha kitu kuelekea kwenye mkusanyiko wa wakristo waliokuwepo kwenye ibada.
Taarifa zinaeleza kuwa eneo kubwa limetapakaa damu, watu wengi wamejeruhiwa. Inasadikiwa kuwa wapo waliokufa lakini haijathibitika. Muda huu vyombo vyote vya usalama vipo eneo la tukio.
Kwa update zaidi sikiliza Radio Mariahttp://streema.com/radios/play/6848.
Hivi sasa kuna taharuki kubwa, na kuna taarifa ya milipuko mingine, haijulikani kama ni ya washambuliaji au ya polisi, mbali na eneo la ibada.
Nawapeni pole nyingi waliokumbwa na mkasa huu, wakatoliki, wakristo wote na wanaolitakia amani Taifa letu.
Taarifa kutoka mkoani Arusha ambazo mtandao huu umezipata zinaeleza kuwa kuna mlipuko mkubwa mfano wa bomu umejitokeza katika kanisa la RC Arusha na kujeruhi baadhi ya waumini.
Mlipuko huo unadaiwa kusababisha taharuki kubwa katika mji wa Arusha na kuendelea kuiweka nchi katika hali tete zaidi .
mwandishi maalum wa mtandao huu kutoka Arusha anasema kuwa tukio hilo limetokea katika parokia ya Olasit mjini Arusha na bado jitihada za uokoaji zinaendelea kufanyika.
Thursday, May 02, 2013
SPOTTED ...........................................................

Bollywood royalty: Veteran actor Amitabh Bachchan celebrated his role in "The Great Gatsby" at the New York premiere on Wednesday, joined by wife Jaya Bhaduri
WAZIRI MKUU AHANI MSIBA WA MZEE ALFRED TANDAU
Waziri mkuu MH. KAYANDA MIZENGO MPINDA Akitia saini kwenye kitabu cha kumbukumbu ya maombolezo ya Kifo cha MH.MZEE ALFRED TANDAU nyumbani kwa marehemu Magomeni Mapipa
MH.Waziri Mkuu akiteta jambo na mtoto wa kwanza wa Marehemu Nd. Julius Tandau
MH.Waziri Mkuu akiteta jambo na mtoto wa kwanza wa Marehemu Nd. Julius Tandau
Wednesday, May 01, 2013
Tuesday, April 30, 2013
MISA YA KUIOMBEA TANZANIA HAPA UK

Wadau mbalimbali Kutoka kushoto Abu Faraji, Caroline Chipeta, Miriam Mungula na Mussa Kabunga baada ya ibada.

Chris Lukosi na Mohsin


Bendara yetu ikipepea

Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Balozi Peter Kallaghe akisalimiana na kiongozi wa kanisani la westmaster abby

Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Balozi Peter Kallaghe akiwa na Frank Eyembe

Wadau mbalimbali waliyojitokeza kwenye ibada
--
Salaam,
Urban Pulse Creative inakuletea taswira kutoka Westminister Abbey jijini London katika misa maalum ya kuombea amani nchi yetu ya Tanzania siku ya muungano iliyofanyika ijumaa tarehe 26.4.13.
Balozi wetu Mh Peter Kallaghe, maofisa kutoka ubalozini na baadhi ya watanzania waishio nchini Uingereza walijumuika pamoja kuhudhuria ibada hii maalum na raia wengine kutoka nchi mbalimbali. Ibada ilianza kwa jumuiya ya Abbey kuwaombea watanzania wote, viongozi pamoja na wanadiplomasia wote waliopo duniani na kwa ajili ya kazi maalum ya Ubalozi wetu hapa nchini Uingereza.
MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU WABARIKI WATANZANIA
Subscribe to:
Posts (Atom)






























