Monday, 9 November 2009

LADYZZZZZZZZZ...

Singer Frenchie Davis and actress Kim Coles attended the 12th Annual GLAAD Tidings Season’s Greenings with Kim in a figure flattering all black outfit punctuated by a sequin tank, and Frenchie in a peachy pink wrap dress and gold sandals. Kim looks hot and sophisticated in her chic outfit and bow front sandals, but hmm, Frenchie…I don’t think the peak-a-boo lace bra works here. She certainly look saucy, but perhaps this dress would have benefited from either a lower cut bra or a cute comfy camisole.

KIPANYA ......................







UMEME WA IPTL WAINGIZWA KWENYE GRIDI YA TAIFA

HATIMAYE mtambo mmoja kati ya mitambo 10 ya Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), umewashwa na kuanza kuingiza mewagati za umeme 10 katika gridi ya Taifa.Akizungumza Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo, Dk. Magesvaran Subramanian, alikiri kuwashwa kwa mtambo huo na kuongeza kuwa uliwashwa rasmi jana saa 6.04 mchana.“Tumeanza kufanya kazi na mtambo mmoja namba moja ndio uliowashwa na mpaka sasa kila kitu kinakwenda vizuri tunatarajia mpaka kesho (leo), utakuwa umeshaanza kuzalisha megwati zote kumi,” alisema Dk. Subramanian.Naye Mfilisi wa kampuni hiyo, Rugonzibwa Mujunangoma, alisema mtambo huo uliwashwa jana, lakini kwa wakati ule haukuweza kuzalisha umeme wote wa megawati 10 na kwamba kadri ulivyokuwa ukiendelea kuzalisha umeme, ndipo megawati zilipokuwa zikiendelea kupanda na kufika 10.“Tangu mtambo uwashwe na hadi ninaondoka muda wa saa saba mchana, mtambo tayari ulishaanza kuingiza megawati 1.5, lakini hadi kesho (leo)), utakuwa tayari unazalisha megawati kumi, ikumbukwe hii ni mashine,” alisema Rugonzibwa.Kuhusu mitambo mingine tisa, alisema mafundi na watalaamu wa masuala ya umeme wanaendelea na ukaguzi ambapo nayo haitochukua muda mrefu itawashwa wakati wowote.“Kuwaka kwa mtambo huu ni dalili nzuri kuwa mitambo mingine nayo haitochukua muda itawaka, mafundi wanaendelea vizuri na kazi yao na kwa kweli hali inatia matumaini,” alisema mfilisi huyo.Kampuni hiyo ya IPTL ina mitambo 10 ambayo kila mmoja ukiwaka utatoa megawati 10 na hivyo mtambo mzima wa IPTL unatarajiwa kutoa megwati 100, na hivyo kupunguza tatizo la mgawo wa umeme ambalo limeikumba nchi kutokana na kuharibika kwa mitambo ya Kihansi na Songas.Rais Jakaya Kikwete aliagiza katikati ya mwezi uliopita kwa mamlaka husika kuwa mitambo hiyo ya IPTL iwashwe ifikapo Novemba mosi, mwaka huu ili kukabiliana na tatizo la mgawo. Imechelewa kuwashwa kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kuchelewa kwa malipo kwa taasisi zitakazohusika kuendesha mitambo hiyo.

Sunday, 8 November 2009

USIKU WA MAGITAA CLUBAFRIQUE

LEO USIKU WA JUMAPILI VIJANA WA "SOUND AFRIQUE BAND" KAMA KAWAIDA WATABURUDISHA KUANZIA SAA 4 USIKU HADI SAA TISA MAJOGOO KATIKA UWANJA WAO WA NYUMBANI 147 BARKING ROAD,CANNING TOWN, LONDON E16 4HQ

MOTO WATEKETEZA "MAISHA CLUB" OYSTERBAY

Kiota cha kujiachia cha Maisha Club kilichopo Oysterbay jijini Dsm leo mchana kimeteketea kwa moto, taarifa zilizopatikana kutoka kwa mashuhuda wamesema kuwa kulikuwapo na ukarabati uliokuwa unaendelea wa vipupwe (AC),kwa bahati mbaya wakati wa ukarabati huo mojawapo ikalipuka kutokana na nyaya zake kugusana,na baadaye moto mkubwa ukazuka katika jengo hilo,imeelezwa kuwa taarifa zilifika kwa watu wa zima moto lakini hawakuwahi kuuzima moto huo kwa haraka kwani kwa asilimia kubwa vitu vilivyokuwemo vilikuwa vimekwishateketea.

Saturday, 7 November 2009

MAZISHI YA MZEE ALEX KUSAGA KATIKA PICHA

















Friday, 6 November 2009

HOUSE FOR SALE

Price: $ 250,000.00
ResidentialSytle: Cottage/BungalowYear Built:
Address: Kijitonyama, Dar es salaam,Dar-es-Salaam, Tanzania
Comm: Negotiable%
Contact:Mtaita+255-773-479555+255-222-700577

WITO SHELUKINDO ATUTOKA DUNIANI

WITO SHELUKINDO AMEFARIKI DUNIA LEO ASUBUHI BAADA YA KUUGUA KWA MUDA MFUPI .KILIO KIKO KIMARA KWENYE NYUMBA YA FAMILIA .MWENYEZI MUNGU AMPE PUMZIKO LA AMANI NA AMWANGAZIE MWANGA WA MILELE MAREHEMU.

KWA HABARI ZAIDI WASILIANA NA
BARAKA SHELUKINDO +255 784 888765

KIMWANA WA WIKI


MALUMBANO CCM

MALUMBANO makali yameendelea kuitikisa Kamati ya rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi baada ya makombora ya juzi kuelekezwa kwa Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango na mumewe, mzee John Malecela.
Kamati hiyo imekuwa ikipokea mashambulizi makali baina ya wabunge ambao wanaonekana kuwa vinara wa vita dhidi ya ufisadi na wale ambao wanaona kuwa vita hiyo inawalenga, kiasi cha kurushiana tuhuma nzito zilizo na mwelekeo wa kuchafuana.
Baada ya kulipuana Jumanne, juzi ilikuwa zamu ya Mama Kilango na mumewe Malecela wakati Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba alipotoa tuhuma nzito akidai kuwa wawili hao pia wamekula fedha za ufisadi.

Habari kutoka vyanzo vyetu zilieleza kuwa Simba alidiriki kudai kuwa hata harusi ya makamu huyo wa zamani wa CCM na Kilango ilifadhiliwa na mtuhumiwa wa ufisadi, Jeetu Patel.
Patel kwa sasa ana kesi katika Mahakama ya Kisutu akituhumiwa kuiibia Benki Kuu (BoT) kwa kuchota takribani Sh11 bilioni kutoka katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA).
Akijieleza kwenye kamati hiyo, Simba alimtuhumu Malecela, ambaye aliwahi kuwa waziri mkuu katika serikali ya awamu ya kwanza, kuwa wakati akiwania kuteuliwa kugombea urais kwa tiketi ya CCM mwaka 2005, Jeetu Patel alimpa Sh200 milioni kwa ajili ya kampeni zake.
Malecela, ambaye wakati huo alikuwa makamu mwenyekiti wa CCM, aliondolewa mapema kwenye mbio za urais, ikiwa ni mara ya pili baada ya kuenguliwa tena mapema mwaka 1995.
Waziri huyo mwenye dhamana ya utawala bora akiwa na taasisi nyeti kama Takukuru na Idara ya Usalama wa Taifa, alizidi kurusha makombora kwa wanandoa hao, akisema Mama Kilango ni mnafiki na sio msafi kiasi cha kuwanyooshea wengine vidole wakati harusi na kampeni zake za ubunge zilifadhiliwa na mtuhumiwa huyo wa ufisadi.
Habari zinasema kuwa Mama Simba alikuwa akizungumza kwa kujiamini na kwa ujasiri na kumtuhumu Mama Kilango kuwa kelele zake zote zinatokana na nongwa ya “kuukosa U-first lady (kuwa mke wa rais).
Alieleza kuwa kelele zote za mbunge huyo wa Same Mashariki zinatokana na chuki na uchu wa madaraka na si kweli kwamba ni mpinga ufisadi, kwa mujibu wa mtoaji habari wetu.
Lakini Patel, alipoulizwa kuhusu tuhuma hizo za Waziri Simba kwamba alifadhili harusi ya Malecela na kampeni zake za urais, alionekana kustuka na kusema: "Haa...we nani kakwambia... Bwana ehee, mimi sijui lolote kuhusu hayo.
"Kwa sasa mimi najiangalia mwenyewe, nina matatizo yangu mengi nahangaika nayo."
Hata alipofafanuliwa kwamba, maneno hayo yalisemwa na Waziri Simba, alijibu: "Kama wao wamesema wenyewe huko, mimi sijui."
Naye Kilango alisema alishuhudia wakati wakati makombora hayo yakirushwa na kueleza kwamba anajiandaa kujibu mapigo.
Mbunge huyo machachari alisema anajua kwamba mambo yote yaliyosemwa, yanamlenga yeye na si mumewe Malecela.
"Mimi ni mwanasiasa... andikeni yote yaliyozungumzwa bila ya kuacha baadhi na siwezi kuwashtaki," alisema Kilango.
Mzee Malecela hakutaka kuzungumzia lolote kuhusu tuhuma hizo wakati alipoulizwa juu ya uhusiano wake na Patel na kama aliwahi kupokea kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya kampeni.
"Ahaa... kijana naomba uniache nipumzike," alisema Malecela.
Mbali na mzee Malecela na mkewe, Waziri Simba pia alimgeukia mwenyekiti mtendaji wa IPP, Reginald Mengi akimtuhumu kuwa anaendesha vyombo vya habari vinavyoichafua CCM na serikali yake kwa maslahi yake binafsi.

Pia alimshambulia mbunge wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe na mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka, akiwatuhumu kuwa ni watu wenye njaa na kwamba, wanalipwa fedha kufanya kazi hiyo.
Waziri Simba alisema kuwa hata tuhuma dhidi ya mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge na mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, zimetokana na chuki binafsi.
Simba alisema kuwa uchunguzi wa kashfa ya rada ulishamalizika na Chenge akasafishwa na kuongeza kwamba hata uchunguzi wa Richmond umebaini kulikuwa hakuna rushwa, kwa mujibu wa mtoaji habari wetu.
Suala la Richmond liliibuka tena mbele ya kamati hiyo ya Mwinyi wakati mbunge wa Bukoba Vijijini, Nazir Karamagi alipolalamika kuwa ripoti ya kamati teule ya Bunge iliyoozwa Dk Mwakyembe haikumtendea haki.
habari hizo toka ndani ya kikao hicho zinaeleza kuwa Karamagi alisema ripoti ya Richmond ilionea baadhi ya watu na akapendekeza iundwe tume huru kupitia mchakato huo kuona kama wana makosa ili haki itendeke.
Mbunge huyo ambaye alijiuzulu uwaziri baada ya Lowassa kuachia wadhifa wake wa waziri mkuu kutokana na kashfa hiyo, alisema maamuzi yake kuhusu Richmond yalitokana na mapendekezo ya Bodi ya Tanesco.
Naye Dk Mwakyembe alijibu hoja iliyotolewa Jumanne na mbunge wa Ukonga, Dk Makongoro Mahanga aliyedai kuwa ripoti ya Richmond ni 'feki', akisema tatizo la Dk Mahanga ni uelewa mdogo.
Kuhusu hoja ya Karamagi, Dk Mwakyembe alisema malalamiko yake si sahihi kwa sababu yapo maeneo mengi ambayo Karamagi alishiriki na yako bayana hayahitaji mjadala.
Aliwatahadharisha Wabunge kuacha kudodosa sana ripoti ya Richmond kwani watazidi kumchafua Lowassa na kwamba wanaweza kufungwa kwa sababu upo ushahidi dhahiri.
Dk Mwakyembe aliwataka viongozi wa CCM wenye tuhuma kuiga mfano wa Mzee Mwinyi aliyejiuzulu baada ya mauaji yaliyofanywa na vyombo vya dola mkoani Shinyanga.
Akizungumza mbele ya kamati hiyo, kwa mujibu wa vyanzo vyetu, alimshambulia spika wa Bunge, Samuel Sitta akidai kuwa kama si mizengwe, suala la Richmond lingemalizwa kwa taratibu za kichama.
Habari hizo zinadai kuwa Chenge, aliyewahi kuwa mwanasheria mkuu wa serikali, alisema Lowassa alizungukwa na kwamba kulikuwa na njama za kummaliza ingawa hakusema njama hizo zilifanywa na nani.
Chenge aliitetea serikali ya awamu ya tatu kuhusu kuingia mikataba mibovu na kusisitiza hakukuwa na uzembe kwani mikataba yote ilipitiwa na kukubaliwa na Baraza la Mawaziri.
Hata hivyo, mbunge wa Muleba Kusini, Wilson Masilingi alisimama na kuomba kutoa taarifa na kumwomba Mzee Mwinyi na kamati yake wawabane wabunge wanaodai wanasema ukweli.
Masilingi alipinga maelezo ya Chenge kuhusu mikataba na kusisitiza kuwa maelezo yake yalijaa ushabiki na kusema Baraza la Mawaziri liliridhia mikataba kutokana na ushauri wake (Chenge).
Mbunge wa Kwela, Dk Chrisant Mzindakaya, ambaye aliwahi kupata umaarufu kwa kulipua kashfa, aliwataka wabunge wakubali matokeo kuhusu Ripoti ya Richmond ili taifa lisonge mbele badala ya malumbano yasiyokwisha.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu, Mzindakaya aliwataka wabunge wafahamu kuwa ripoti hiyo ilishapitishwa na Bunge na haiwezi kurejeshwa ianze tena upya.
Naye Dk Mlingwa (Shinyanga Mjini), alisema mpasuko unaoinyemelea CCM unatokana na chama hicho kuacha misingi yake ya kuwa chama cha wakulima na wafanyakazi na badala yake kinawakumbatia wafanyabiashara.
Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Emanuel Nchimbi alitumia nafasi yake kuomba maridhiano ya wabunge wa CCM, kujenga moyo wa kusameheana ili chama kisonge mbele.

Thursday, 5 November 2009

KATUNI YA LEO


Wednesday, 4 November 2009

BARAFU KUYEYUKA MLIMA KILIMANJARO

Wanasayansi kutoka Marekani wamegundua kuwa theluji na barafu katika mlima mrefu barani Afrika, Kilimanjaro uliopo nchini Tanzania inayeyuka kwa kasi na huenda ikatoweka ndani ya miaka 20.Utafiti huo ambao umechapishwa katika jarida la Proceedings of the National Academy of Sciences, ulikuwa wa kwanza kujua kiwango cha barafu kilichopotea katika mlima huo. Umegundua kuwa tandiko kuu la barafu hiyo lilisinyaa kwa asilimia themanini na tano tangu mwaka 1912.Barafu nyingine ilisinyaa kwa zaidi ya asilimia hamsini katika kipindi cha miaka tisa iliyopita.
Utafiti huo umebaini kuongezeka kwa joto la dunia huenda ikawa ndio sababu ya kuyeyuka kwa theluji hiyo.

KESI YA KINA MRAMBA -RAIS MSTAAFU ATAJWA

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam jana ilielezwa kuwa Rais mstaafu Benjamin Mkapa ndiye aliidhinisha mchakato wa kuiajiri Kampuni ya Alex Stewart uendelee kwa haraka.
Hayo yalielezwa mbele ya jopo la mahakimu watatu lililokuwa likiongozwa na hakimu John Utamwa wakati Wakili Hurbet Nyange alipokuwa akimhoji shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka Godwin Nyelo (48).
Nyelo ambaye alikuwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Sheria na masuala ya Uchumi wa Wizara ya Nishati na madini ni shahidi wa kwanza kwa upande wa mashtaka kutoa ushahidi wake katika kesi ya kutumia madaraka vibaya na kuisababishia hasara ya zaidi ya Sh 11 bilioni serikali inayowakabili Mramba, Daniel Yona na Katibu Mkuu mstaafu wa Wizara ya Fedha na Uchumi Gray Mgonja.
Hata hivyo shahidi huyo alisema Rais Mkapa alihusika katika kukubali mchakato huo uendelee haraka baada ya Wakili Nyange kumuonyesha dokezo na kumtaka asome sehemu ya dokezo hilo naye kufanya hivyo mahakamani hapo.
Dokezo hilo lilikuwa limeandikwa kutoka kwa Daniel Yona ambaye kwa wakati huo alikuwa Waziri wa Nishati na Madini kwenda kwa Rais huyo wa serikali ya awamu ya tatu.

HERE & THERE ...




Tuesday, 3 November 2009

MZEE ALEX KUSAGA AFARIKI DUNIA


Mwenyekiti mtendaji wa Clouds Media Group,Bw Alex Kusaga ambaye ni baba yake mzazi na Joseph Kusaga,amefariki leo jioni nchini Afrika ya Kusini ambako alipelekwa kwa ajili ya matibabu. Kwa taarifa zaidi tutaendelea kuwajulisha kadiri ya zitakavyokuwa zinatujia.

MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI-AMIN

HOSEAH AKOLEZA MOTO

MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah amekoleza moto wa mjadala wa Bunge kuhusu utendaji wa taasisi yake baada ya kujitokeza hadharani na kueleza kuwa hana mpango wa kujiuzulu.
Na kama haitoshi, Dk Hoseah amesema wabunge hawamtaki, wapige kura za kutokuwa na imani naye, ikiwa ni siku mbili kabla ya Bunge kujadili taarifa ya serikali ya utekelezaji wa maazimio ya chombo hicho kesho, kama alivyoahidi Spika Samuel Sitta.
Katika maazimio hayo kuhusu kashfa ya utoaji umeme wa dharura kwa kampuni ya Richmond Development LLC, Dk Hoseah anatakiwa kuwajibishwa na mamlaka ya juu kutokana na taasisi yake kushindwa kubaini rushwa katika utoaji wa zabuni hiyo.
Hoseah, aliyeitisha mkutano na waandishi wa habari ambao kila mmoja alipewa kipeperushi kinachotoa ufafanuzi wa athari za malipo yasiyostahili kwa watumishi wa umma na adhabu zake, alionekana ni mwenye jazba, msimamo na kujiamini, licha ya joto la uchunguzi huo na shinikizo la wabunge kutaka awajibishwe, kuwa juu.
Akijibu swali kwamba kwanini asijiuzulu ili kuonyesha uadilifu baada ya maafisa wenzake waandamizi wa serikali waliotajwa katika Richmond kung'oka, Dk Hoseah alianza kuhoji: "Kwanini unataka nijiuzulu.
"Sasa nakwambia, sina mpango wa kujiuzulu siwezi kujitia kamba eti ili nionekane mzalendo bila kosa, kwanini unataka nijiuzulu au unataka kuchukua nafasi yangu?"
Hadi sasa, serikali haijaeleza kama imeshawashughulikia maofisa waandamizi waliotakiwa kuwajibishwa na mamlaka za juu, lakini katika kipindi cha miezi michache iliyopita, aliyekuwa Mwanasheria Mkuu Johnson Mwanyika na Arthur Mwakapugi, aliyekuwa katibu mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini walistaafu kwa mujibu wa sheria.
Kauli ya Dk Hoseah inakuja wakati Takukuru ikishutumiwa kuwa inaendesha uchunguzi kuhusu malipo ya posho mbili dhidi ya wabunge kwa lengo la kuwashughulikia wale ambao wamekuwa mstari wa mbele kutaka serikali imwajibishe kutokana na uhusika wake kwenye kashfa ya Richmond.
Kashfa hiyo ya Richmond tayari inaonekana kusababisha msuguano mkubwa kati ya Bunge na Serikali, kiasi cha kusababisha watendaji wakuu wa taasisi hizo kutofautiana misimamo.
Huku kukiwa na ongezeko la kilio cha kutaka awajibishwe, Dk Hoseah alisema: "Nihukumiwe kwa haki si kwa hisia. Kosa langu nini katika Richmond, taarifa ya pili ya azimio namba 20 la Kamati ya Nishati na Madini bungeni iko wazi... lakini nasema uchunguzi dhidi ya wabunge utaendelea na naomba watoe ushirikiano; waiache Takukuru ifanye kazi zake; waonyeshe uongozi wa mfano na uadilifu kama ambavyo wamekuwa wakipambana na ufisadi."
Kumbukumbu za Bunge (Hansard), kuhusu Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini ya Agosti mosi, kujibu taarifa ya serikali iliyotolewa Julai 25, inasema: "Mheshimiwa Spika, Azimio Na. 20, Serikali iendeshe uchunguzi maalum ili kubaini ukweli kama taarifa rasmi ya Takukuru iliyotoa matokeo ya uchunguzi kuhusu mchakato wa Richmond ilikataliwa na kuharibiwa na kutolewa nyingine.
"Na kama jalada halisi linalohusu kampuni ya Richmond lililokuwa BRELA liliharibiwa na kuwekwa jingine kwa lengo la kuficha ukweli. Mheshimiwa Spika, Utekelezaji wa Serikali: Kamati ya Vyombo vya Dola imekamilisha uchunguzi wake kuhusiana na suala hili.
"Na imebainika kuwa, si kweli kuwa taarifa rasmi ya Takukuru iliyotoa matokea ya uchunguzi kuhusu mchakato wa suala la Richmond ilikataliwa na kuharibiwa na kutolewa nyingine kwa lengo la kuficha ukweli.
"Vile vile, taarifa ya kamati ya vyombo vya dola inaonyesha baada ya upelelezi na uchunguzi wa kina kufanyika wameridhika kuwa jalada halisi la Richmond lililokuwa BRELA halikuharibiwa na wala hakukuwa na jalada lingine lililowekwa kuficha ukweli wa jambo hili."
"...Maoni ya Kamati; Kamati inaridhika na taarifa hiyo."
Hoseah akitumia azimio hilo, alisema alibahatika kusoma kwa makini taarifa zote za kamati kuanzia ya kwanza na hiyo ya pili na kuhoji : "Sasa nijiuzulu kwa kosa lipi, watu mnihukumu kwa haki, au unataka kuchukua nafasi yangu (alimuuliza mwandishi wa gazeti hili)?"
Alisema kwa kipindi chote atakachokuwepo katika uongozi, atasisimamia sheria na hakuna aliye juu ya sheria na kuongeza: "Watu waache danganya toto, hakuna kisasi ni usimamizi na utekelezaji wa sheria tu."
Dk Hoseah alifafanua kwamba, tayari suala hilo la kuwajibishwa liko mamlaka ya juu (rais), hivyo ni vema wakasubiri maamuzi na kusisitiza kwamba, "uchunguzi huo utaendelea kwa hiyo waheshimiwa wabunge, wazee wangu toeni ushirikiano ili suala hili lisije kutufikisha pabaya, nchi hii ni ya amani".
Mkuu huyo alitumia mkutano huo kufafanua pia kwamba, uchunguzi huo haukumlenga mtu yeyote ambaye ni mjumbe wa kamati iliyochunguza kashfa ya Richmond, akisema: "Kwanini, mbona Mheshimiwa Zitto (Kabwe) tumemhoji, yeye alikuwa kamati ya Richmond?"
Hoseah alisema ombi la kufanywa uchunguzi huo ni la Bunge lenyewe kupitia barua ya Februari 26, 2008, ambayo ilimtaja yeye kwa jina ikimtaka afanye uchunguzi huo na kuhoji: "Kwa hiyo Bunge lenyewe linaweza kuandika barua kutaka kuwalenga watu fulani?"
Spika Sitta alishaeleza kuwa hafahamu lolote kuhusu uchunguzi huo na kuitaka serikali isitishe zoezi hilo, huku Waziri Mkuu Mizengo Pinda akieleza kuwa suala hilo linatokana na maagizo ya ofisi ya rais.
Hata hivyo, alisisitiza kwamba kinachofanyika ni uchunguzi na haimaanishi wabunge wamethibitika kula posho mara mbili na kuongeza: "Sasa si ndiyo vizuri,... kwanza tunawapa haki nao kuwasikiliza, maana inawezekana mwisho wa siku ikibainika ni taarifa feki."
Kuhusu malalamiko ya wabunge kudhalilishwa na kuhojiwa na vijana wadogo wa taasisi hiyo, alipinga akisema si kweli na kuongeza: "Afisa ambaye anasimamia jambo hili ni mchunguzi mkuu ambaye amekuwa katika fani hii tangu mwaka 1973... kwa umri alionao hadi sasa anatarajia kustaafu mwakani."
Hata hivyo, awali akijibu maswali mengine, kama tatizo ni baadhi ya wabunge hawataki kuona sura yake (Hoseah) basi ni vema wakapiga kura ya kutokuwa na imani naye.
"Kama ulivyosema tatizo ni Hoseah hawajadili Takukuru, basi kama hawataki kuona sura yangu wapige kura ya kutokuwa na imani na mimi," alisisitiza.

UMALKIA WA KISURA TANZANIA


Visura wanaowania Umalkia wa Kisura wa Tanzania, juzi waliingia kambini katika hoteli ya Kiromo iliyopo Bagamoyo mkoani Pwani wikiendi hii na kupokelewa kwa shangwe na wenyeji wao. Akizungumza hotelini hapo, Meneja Mradi wa kampuni ya Beautiful Tanzanie Agency, Grace Kilembe, washiriki hao walipatikana kutoka katika mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara. Aliitaja mikoa iliyofanyiwa usaili na kuwapata washiriki hao walioingia kambini juzi ni Singida, Dodoma, Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Arusha, Mara na Dar es Salaam ambapo waliwapata wasichana 20 wenye vigezo vya mashindano hayo.


Aliwataja wasichana hao na mikoa waliyotoka kwenye mabano ni Mwajabu Juma (Mwanza), Lucky Mwakatobe, Resson Soto (Arusha), Jack's Oyombe, Alinda Lema, Violet Mganga, Sharon Silas (Dar es Salaam), Jackline Benson (Arusha) na Gloria Gilbert (Tanga). Wengine ni Glady Molel, Lightness Mwanga, Mwatatu Francis, Mary Joel, Shamim Babu (Manyara) na Mary Mallya (Dodoma), Asnat Mohammed na Diana Ibrahim (Mara).


Alisema washiriki hao watakaa katika kambi kwa muda wa mwezi mmoja na wiki mbili huku wakitoka mmoja mmoja mpaka watakapobaki 10 ambao wataingia fainali ya mashindano hayo. Grace alisema visura 10 watakaoingia fainali hiyo watapatikana kwa njia ya kupigiwa kura na watazamaji wa televisheni ya TBC1.


Mashindano ya Kisura wa Tanzania yamedhaminiwa na Serengeti Breweries Limited (SBL), Kiromo Resort, TBC1, Clouds FM, FHI, ATC, Entertainment Masters, Mwananchi Communication, Hugo Domino, Mercy G Parlor Beauty na Bang! Magazine. Grace alisema mwaka huu walijitokeza visura wengi katika hatua za awali tofauti na mwaka jana na kuwapa moyo waandaaji hao kuwa, wengi wameanza kuyaelewa mashindano hayo na manufaa yake.

Monday, 2 November 2009

HAFLA YA SOMESHA MTOTO WA KIKE MLIMANI CITY...











Sunday, 1 November 2009

KATUNI YA LEO


Saturday, 31 October 2009

KIMWANA WA WIKI


SIMBA 1 YANGA 0

SIMBA YA MSIMBAZI LEO HII IMEFANIKIWA KUWAFUNGA MAHASIMU WAO WAKUBWA YANGA KWA BAO 1 KWA 0
Habari zaidi tembelea www.issamichuzi.blogspot.com

SIMBA NA YANGA UWANJANI LEO


Macho na masikio ya maelfu ya mashabiki wa soka nchini leo yataelekezwa kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya soka ya Tanzania Bara kati ya vigogo vya soka hapa nchini Simba na Yanga.
Huo utakuwa ni mchezo wa pili kwa vigogo hivyo kukutana ndani ya mwaka huu, ambapo mara ya kwanza ilikuwa ni Aprili 19 katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja huo na timu hizo kwenda sare ya 2-2, ambapo Yanga ilikuwa na jukumu la kusawazisha.
Mchezo wa leo utakuwa na umuhimu mkubwa kwa Yanga kutokana na ukweli ina changamoto kadhaa za kukabiliana nazo.
Kocha mpya, Kostadin Papic aliyechukua mikoba kutoka kwa Dusan Kondic atakuwa anakalia benchi la timu hiyo kwa mara ya kwanza wiki tatu zilizopita.
Pia Yanga yenye pointi 18 itakuwa na kibarua cha kupunguza kasi ya Simba, ambayo inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 27 baada ya kushinda mechi zake tisa za mwanzo.
Kutokana na ukweli kuwa ikipoteza mchezo huo ina maana itazidi kutoa mwanya kwa Simba kuzidi kupaa katika msimamo wa ligi hiyo. Yanga itakuwa fursa kwao kuendeleza ubabe wa kuifunga Simba kwa mara ya pili kwenye uwanja huo kama ilivyofanya katika raundi ya kwanza ya Ligi Kuu msimu uliopita, ambako Yanga ilishinda bao 1-0, Oktoba 26,2008.
Katika mchezo huo, Simba itakuwa na kazi moja tu ya kuhakikisha wanaendeleza wimbi la ushindi kwenye michezo yake ya ligi pamoja na kutaka kuweka rekodi mpya ya kushinda michezo 10 mfululizo.
Akizungumzia mchezo huo, kocha wa Yanga, Kostadin Papic alisema kuwa mara baada ya kukirekebisha kikosi chake ana matumaini ya kufanya vizuri kwenye mchezo huo.
Kwa upande wake, kocha wa Simba, Patrick Phiri aliweka wazi kuwa anachohitaji ni pointi tatu kutoka kwa Yanga na uhakika wa kuzipata pointi hizo anao.

Friday, 30 October 2009

KLABU MPYA YA KISASA KUFUNGULIWA USIKU HUU




LEO USIKU KUANZIA SAA TATU KLABU MPYA YENYE KUMBI TATU PAMOJA IKIWEMO RESTAURANT ITAKAYOJULIKANA KAMA "CLUB AMBASSADOR" INAFUNGULIWA RASMI JIJINI LONDON MAENEO YA BARKING ADDRESS KAMILI NI:
20-30 LONDON ROAD
BARKING
IG11 8AG

MAWASILIANO:
JIMMI 0787 418 534
JOHN 07529 410 125
KARIBUNI NYOTE

Thursday, 29 October 2009

AISEE ! KANYE TAFADHALI MaZEE



WANAWAKE WA TANZANIA KATIKA GOLF

Wachezaji wa timu ya taifa ya wanawake ya mchezo wa Golf, wakiwa wameshikilia makombe na ngao walizofanikiwa kuzibeba baada ya timu hiyo kuibuka mabingwa wa mashindano ya Afrika mashariki na Kati yaliofanyika Kampala , Uganda . Jumla ya nchi tano zilizoshiliki katika mashindano hayo ambazo ni Tanzania , Kenya , Zambia , Rwanda na wenyeji Uganda .

NANI AMETOKA ZAIDI ?

Rihanna na Melody Thornton wakiwa wamevalia viatu vinavyoishia mapajani, ubunifu toka kwa Muingereza Stella McCartney .

AMANI LEO


KUMBUKUMBU (SIMBA SPORTS CLUB)

1) Mackenzie Ramadhani
2) Mavumbi Omari
3)Twaha Hamidu
4)Deo Njohole
5)George Masatu
6) Iddi selemani
7) Zamoyoni Mogella
8)Malota Soma"ball juggler"
9) Hamis Gaga "gagarino"
10) John Makelele
11)Raphael Paul

WADAU TUNAOMBA FIRST ELEVEN YA YANGA ENZI HIZO TUICHAPISHE PIA TIMU YA TAIFA ILOENDA LAGOS MIAKA YA THEMANINI KATIKA KOMBE LA MATAIFA HURU YA AFRIKA ENZI ZA PETER TINO

MISS TOURISM ILALA WAPEWA MIL.50

Mwandaaji wa Miss Tourism Ilala 2009 Amina Boka wa pili kutoka kulia akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Savannah Lodge katika Hoteli ya City Paradise Mchana huu wakatika kampuni ya Chicken Hunt ambayo ni kampuni mama ya Savannah Lodge na Kampala Unirvesity ilipotangaza udhamini wa shilingi Milioni 50 kwa shindano hilo linalotarajiwa kufanyika Novemba 6 kwenye ukumbi wa Dar West Tabata jijini Dar es salaam.

MASTAA WA KIKE NA TABASAMU

Kim Kardashian
Aunt Ezekiel(kulia) na Aisha Bui

Monday, 26 October 2009

MTOTO WA AJABU

Mtoto Ali Yakubov mwenye umri wa miezi tisa amepata umaarufu mkubwa na amekuwa gumzo dunia nzima baada ya taarifa za miujiza yake ambapo maneno tofauti tofauti ya kiarabu kuanza kutokea kwenye mwili wake.

Maandishi ya kiarabu yanayonukuu aya za Quran yamekuwa yakitokea kwenye mikono yake, miguu na tumboni na kisha kutoweka baada ya siku kadhaa na kisha maandishi mengine ya kiarabu yanayonukuu vipande tofauti vya aya za Quran hujitokeza upya.Madaktari nchini Urusi hadi leo bado hawajui nini kinaendelea kwenye mwili wa mtoto huyo ambaye maandishi ya kwanza ya kiarabu yanayosema neno "Allah" yalijitokeza kwenye kidevu chake ndani ya wiki moja baada ya kuzaliwa.

Awali watu wanaopinga miujiza ya mtoto huyo walianza kuvumisha kuwa wazazi wa mtoto huyo ndio wanaomuandika maneno hayo mtoto huyo lakini madaktari wamepinga uvumi huo na kusema kwamba maandishi hayo si maandishi ya mtu kuandika juu ya ngozi kwani yanatokea toka ndani ya ngozi ya mtoto huyo.Mama wa mtoto huyo, Madina alisema kwamba yeye na mumewe walikuwa si watu wa dini mpaka maandishi hayo yalipoanza kutokea.Awali maandishi hayo yalipotokea hawakutaka kumuonyesha mtu yoyote mpaka walipomuonyesha daktari wao na baadae imamu wa mji wao kuitwa kuangalia maandishi hayo.Hivi sasa mtoto huyo ameufanya mji wa Dagestan, kusini mwa Urusi uwe maarufu sana kwani mamia ya watu kutoka kona mbali mbali duniani wanamiminika kwenye mji huo kumuona na kuomba dua mbele ya mtoto huyo."Huyu mtoto ni dalili tosha ya kuwepo kwa Mungu", alisema mbunge wa mji huo Akhmedpasha Amiralaev na kuongeza "Mungu amemleta Dagestan ili kusaidia kuiokoa jamii yetu".

Mama wa mtoto huyo alisema kwamba kawaida maandishi hayo hutokea mara mbili katika kila wiki, siku ya jumatatu na usiku wa kuamkia ijumaa."Ali husikia maumivu makali wakati maandishi haya yanapoanza kujitokeza, hulia sana na joto la mwili wake huwa juu sana, ni vigumu kumshikilia wakati maandishi hayo yanapokuwa yakitokea kwahiyo huwa tunamuacha kwenye kiti chake", alisema mama wa mtoto huyo.Mama huyo aliendelea kusema kuwa aya tofauti hujitokeza kila maandishi mapya yanapotokea.Imamu wa mji huo Imamu Abdullah amekuwa akiwaambia watu wanaoshangazwa na mtoto huyo kwamba Quran ilishatabiri kuwa kabla ya kiama watatokea watu wenye maandishi ya quran kwenye miili yao.Mojawapo ya maandishi yaliyojitokeza kwenye mwili wa mtoto huyo ni yale yanayosema "Usizifiche dalili hizi kwa watu".

IJUMAA WIKIENDA


SERENGETI BREW. YATOA MSAADA BOMBO HOSPITALI

Meneja uhusiano wa kampuni ya Serengeti Breweriers Teddy Mapunda akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Tanga mjini Bw. Ibrahim Msengi Mashuka na Vyandarua kwa ajili ya Hospitali ya wodi ya wazazi katika Hospitali ya Rufaa ya Bombo.

KATUNI YA LEO

UMEME WA IPTL GHALI KULIKO DOWANS

• Total waleta shehena ya mafuta tani 7,500

• Yataumika kfua umeme megawati 100

• IPTL kutumia Shs milioni 766 kila siku ya Mungu



Shehena ya kwanza ya mafuta kwa ajili ya mitambo ya kuzalisha umeme ya Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) inawasili leo nchini. Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, alisema Dar es Salaam jana kuwa shehena hiyo itakuwa ni ya ujazo wa tani 7,524. Mitambo ya IPTL itawashwa Jumapili ya Novemba Mosi mwaka huu huku uendeshaji wake ukiigharimu serikali Sh. Bilioni 23 kwa mwezi, sawa na Sh milioni 766 kwa siku. Jumanne wiki hii, Rais Jakaya Kikwete aliagiza kuwashwa mara moja kwa mitambo hiyo inayotumia mafuta baada ya nchi kuingia gizani kutokana na kuharibika kwa mitambo ya Songas na Kihansi. Rais aliziagiza Wizara za Fedha na Uchumi , Nishati na Madini, Katiba na Sheria na Shirika la Umeme (Tanseco) kufanya kazi kila moja kwa nafasi yake kuhakikisha mitambo inawashwa. “Hadi jana (juzi) mchakato wa kupatikana mafuta ulikuwa umekamilika. Wizara ya Fedha na Uchumi imeshajipanga kwa ajili ya malipo ya mzigo huo ili kusiwe na mgogoro wowote.” alisema Ngeleja. Alisema kampuni ya Total Tanzania Limited ndiyo iliyopewa dhamana ya kuleta shehena hiyo. “Ile mitambo inawashwa kwa kufuata taratibu maalum na sasa wataalamu wanaendelea na kikao kati ya Tanesco, mfilisi (RITA), Wartsila, benki ya Standard Chartered, wakijadili gharama mbalimbali kama mafuta na kujua zitumie siku ngapi kuipasha moto mitambo.” alisema. Waziri huyo wa Nishati na Madini aliuhakikishia umma kuwa mchakato wa takwimu zote zinazohusu mitambo ya IPTL kuiwezesha inawashwa zimeshwapelekwa tangu jana Wizara ya Fedha na Uchumi kwa ajili ya uhakiki ili fedha iweze kutolewa. Mtambo wa Songas wenye kuzalisha megawati 20 ulitarajiwa kuwashwa jana , huku mtambo wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) wa Hale – Tanga nao ukiwa umeanza kuzalisha umeme wa megawati kati ya 5 na 6 kutokana na kina cha maji ktotosheleza uwezo wa megawati 8. Awali, Kaimu Meneja Uendeshaji wa kampuni ya Wartsila, Gilbert Ndesamburo, aliwaambia waandishi akiwa pamoja na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja kuwa mitambo hiyo, amabyo illingizwa miaka miwili iliyopita, ikiwashwa kwa saa 24 hutumia mafuta lita 625,000 huku lita moja ya mafuta hayo ikiuzwa kwa Sh 1,200. Ndesamburo alisema kituo hicho kina uwezo wa kuhifadhi mafuta kwa wastani wa tani 15,000 sawa na zaidi ya lita milioni 15. Mitambo hiyo, ambayo ipo kumi na yenye uwezo wa kila moja kutoa megawati 10, ilifungwa nchini mwaka 1998 na ikiwashwa hufua megawati 100 za umeme. Serikali ilikuwa imeagiza mitambo hiyo ibadilishwe iwe inatumia gesi asilia kuiendesha , ili kupunguza gharama za uzalishaji, lakini Wizara ya Nishati na Madini ikasimamisha mchakato huo kusubiri kumalizika kwa kesi ya msingi inayoendelea mahakamani. Katikati ya mwaka huu Rais Kikwete aliagiza mchakato huo wa kubadili mitambo uendelee badala ya kusubiri kesi hiyo kumalizika. Uendeshaji wa mitambo ya IPTL kwa sasa unasimamiwa na kuendeshwa na kampuni kandarasi ya Wartsila,ambayo iliingia mkataba wa miaka miwili na serikali, kuendesha mitambo ya kuzalisha umeme. Mwaka 2006 nchi illingia gizani wakati kulipotokea ukame mkubwa na kusababisha serikali kutafuta suluhisho la haraka ambalo lilisababisha ijikute ikiangukia kwenye kashfa ya Richmond. Kiwango kinachotumiwa na IPTL kufua umeme, kinaanza kufungua sura mpya yenye kuonyesha kuwa kazi ya kuzalisha umeme si lelemama inahitaji fedha nyingi ajabu. Itakumbukwa kuwa Kamati ya Bunge ya Kuchunguza Mkataba Tata wa Richmond, ilisema kuwa serikali ilikuwa inaingia gharama kubwa kulipa Sh. Milioni 152 kwa siku kwa ajili ya kuzalisha megawati 125 kupitia Kampuni ya Dowans. Kwa sasa IPTL watalipwa Sh milioni 766 kila siku ya Mungu kama gharama za uendeshaji na watazalisha megawati 100, ikilinganishwa na 125 za Dowans ambazo zingezalishwa kwa h milioni 152 kwa siku. Kampuni ya Songas ambayo inazalisha umeme megawati 180 hupokea Sh milioni 284 kila siku iendayo kwa Mungu tangu ilipoingia mkataba na serikali. Hii inathibitisha kuwa gharama za kuzalisha umeme ziko juu sehemu zote duniani. Tangu Septemba, mwaka huu, nchi iliingia gizani baada ya kuwepo upungufu wa megawati 180 kwenye gridi ya taifa kutokana na kuharibika kwa mitambo ya Hale na Kidatu. Kwa sasa imeelezwa imetengamaa.

Friday, 23 October 2009

MISS LAKE ZONE & MISS TANZANIA AREJEA MWANZA

Vodacom Miss Tanzania Miriam Gerald,akiwapungia mkono wananchi wa jiji la Mwanza walipompokea jana jijini humo, aliyesimama kushoto ni Mwandaaji wa Vodacom Miss Mwanza Flora Lauwo ambaye pia ndiyo mratibu wa mapokezi hayo kupitia kampuni yake ya Flora Talent Promotions. Miriam anatarajiwa kufanyiwa sherehe kubwa leo jioni itakayofanyika katika hoteli ya Nyumbani Hotel iliopo ndani ya jengo la NSSF,jijini Mwanza katika kumkaribisha rasmi ,aidha katika hafla hiyo ya aina yake mgeni wa heshima atakuwa ni mkuu wa Mkoa wa Mwanza Abbas Kandoro.

K'S BAKERY KUFUNGULIWA WIKI IJAYO

KiOTA KIPYA CHA KISASA KATIKA UOKAJI MIKATE NA KEKI NK KINATAZAMIWA KUFUNGULIWA WIKI IJAYO JIJINI DARESSALAAM MMILIKI WAKIOTA HICHO BI.TEDDY KAEGELE AMESEMA HABARI ZAIDI ZIKO NJIANI